Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Friday 30 May 2014

MIGOGORO YA ARDHI YAWA KERO KUBWA MKOANI MANYARA, KINANA AAHIDI KUFUATILIA SUALA HILO

2sKatibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa na vikundi vya ngoma wakati alipowasili katika kata ya Gallapo kijiji cha Ayamango jimbo la Babati vijijini akiwa katika ziara ya kikazi ya kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali na kusikiliza kero mbalimbali za wananchi na kuangalia utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010, Huku akiimarisha uhai wa chama cha mapinduzi. Katika ziara hiyo Kero kubwa iliyochukua nafasi ni ya migogoro ya ardhi ambapo kumekuwepo na uvamizi wa maeneo mbalimbali aidha ya wakulima au wafugaji ama hifadhi, Jambo ambalo limemfanya Katibu huyo Ndugu Abdulrahman  Kinana kuwaambia wananchi hao kwamba atahakikisha anafuatilia suala hilo na kulifikisha kwa Rais Jakaya Kikwete ili aweze kuona ni kwa jinsi gani litatatuliwa kwani yeye ndiyo mwenye mamlaka ya kufuta hati za umiliki wa ardhi kwa mtu au taasisi yoyote. Katika ziara  hiyo Kinana anaongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi na viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali katika  mkoa wa manyara.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-BABATI -MANYARA)1sKatibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa amezingirwa katikati na kikundi cha ngoma wakati akipokelewa alipowasili katika eneo la mkutano uliofanyika katika kijiji cha Amayango kata ya Gallapo.3sAkina mama wakipiga ngoma wakati wa mapokezi hayo.4sKatibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wa tatu kutoka kulia  na baadhi ya viongozi wa mkoa wa Manyara wakiwasili katika eneo la mkutano uliofanyika kijiji cha Ayamango.5SNape Nnauye Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi akiwa amevalia vazil rasmi la kimila la heshima ya wazee wa kijiji cha Amayango.6SWasichana wakiwa wamevalia mavazi ya kiasili.7SBaadhi ya kompyuta zilizokabidhiwa kwa shule mbalimbali na mbunge wa jimbo la Babati vijijini Mh. Jitu Son wakati wa mkutano huo.8SKatibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa amekaa meza kuu pamoja na viongozi wa mkoa wa manyara.9SBaadhi ya wananchi wakiwa katika mkutano huo.11SUmati wa wananchi waliohudhuria katika mkutano huo uliofanyika katika kijiji cha Amayango kata ya Gallapo.12SBaadhi ya wapiga picha wa vyombo mbalimbali wakiendelea na kazi yako ya kuchukua matukio katika mkutano huo.13SMmoja wa wanavijiji waliofika katika mkutano huo Bw.Sumi Mtuka kutoka kata ya Kashi Babati akitoa kero zake mbele ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.15SNaye Bi.Elizaberth Manda mkazi wa kata ya Gallapo akitoa kero zake katika suala zima la ardhi ambalo limekuwa ajenda kubwa katika ziara hiyo hasa kwa wakulima na wafugaji.16SKatibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza kwa makini  Mhandisi wa maji Babati Injinia Emmanuel Konkomo ambaye alitakiwa kueleza sababu za idaya ya maji katika wilaya hiyo kuchukua mradi wa maji ulioanzishwa na wananchi katika kata ya Gallapo na kuanza kuwatoza gharama kubwa za malipo ya bili za maji bila hata ya kukubaliana nao jambo ambalo limelalamikiwa na wananchi hao.17SMhandisi wa maji Babati Injinia Emmanuel Konkomo akijaribu kutoa maelezo kwa wananchi ambao walionekana kutomwelewa na kukubali maelezo yake kutokana na suala hilo kuchukua muda mrefu bila kutatuliwa.18SBaadhi ya wamjengo ya chuo cha walimu wa Sayansi kilichojengwa katika kijiji cha Mamire.19SKatibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipiga picha ya pamoja na viongozi wa taasisi ya Rotary Club ya Babati ambayo imechangia kiasi cha shilingi milioni 50.000 katika ujenzi huo.21SKatibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozwa na mbunge wa jimbo la Babati vijijini Mh. Jitu Son wakati alipokagua ujenzi wa chuo hicho.23SKatibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi katika kijiji cha Amayango.24SNape Nnauye Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi akiwahutubia wananchi katika mkutano huo uliofanyika kijiji cha Amayango.


CHANZO FULL SHANGWE

No comments:

Post a Comment