Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Tuesday 27 May 2014

BARAZA LA MADIWANI ARUSHA LATOA SIKU 30 KUKAMATWA MGANGA MKUU WA JIJI


Na Mwandishi wa brotherdanny5.blogspot, Arusha

Baraza la madiwani Jijila Arusha limetoa siku 30 za kukamatwa kwa aliyekuwa mganga mkuu wa Jiji Dk. Isack Ibrahimu kwa kosa la kutaifisha na kujimilikisha mali za hospitali ya Levolosi ambazo zilitolewa na wafadhili.
Agizo hilo linakuja mara baada ya baraza hilo kubaini kuwa mali ambazo zilikuwa zimetolewa na Hospitali ya KCMC pamoja na FHI hazikukabidhiwa kwa uongozi wa Jiji.
Pia mali hizo ambazo zilitumika kwenye mradi wa utafiti ambao ulikuwa unafanywa chini ya hospitali hiyo na FHI zilipaswa kukabidhiwa kwa uongozi wa Jiji mara baada ya kukamilika lakini daktari huyo alijichukulia mali hizo kama zake
Akiongea kwenye Baraza la Madiwani mapema jana diwani wa kataya levolosi ambapo ndipo mradi huo wa utafiti ulikuwa unafanyika, Ephata Nanyaro alisema kuwa mradi huo ulifanyika kwa masharti maalumu kuwa utakapokamilika vifaa vyote vilivtyokuwa vinatumika basi vitabaki kwenye uongozi wa Jiji.
Nanyaro alisema kuwa watafiti hao waliomba eneo kwa ajili yashuguli zao za utafiti na walidai kuwa eneo ambalo watalirtumia litabaki kama mali ya Jiji pamoja na vifaa vyote lakini kitu cha kushangaza ni kuwa wameshakabidhi tayari mradi kwa Jiji na vifaa havionekani.
Alisema, mradi huo ulikamilika mwaka 2012 mwezi Julai ukiwa na vifaa vingi kama vile magari ambavyo vina thamani ya zaidi ya milioni 700 lakini daktari huyo alihamisha vifaa hivyo huku akiwa anadai kuwa ni mali ya KCMC jambo ambalo sio la kweli.
"Mimi niliona vifaa hivyo vikiwa vinahamishwa ila nilitumia nguvu ilishindikana na sasa nilifanikiwa kuweka kofuli kubwa kwenye jenereta ambayo ndioyoiliyosalimika kwenyeufisadi huo," aliongeza Nanyaro.
Pia alisema kuwa baada ya kufuatilia kwa barua juu ya vifaa hivyo vya mradi wa utafiti wa mama viliovyokuwa  chini ya hospitali ya KCMC walijua kuwa havijarudishwa na KCMC waliwataka viongozi wa jiji warejee kwenye makubalino ya mkataba ambao ulikuwa unasema kuwa kazi yao ya utafiti ikiisha basi wataweza kuwapa jiji majengona vifaa vyote ili nao waweze kunufaikana mradi huo.
Kutokana na hiyo ambayo ilisababisha mtafaruku mkubwa sana kwenye baraza hilo liliamua kutoa siku 30 kwa viongozi kuhakikisha kuwa wamemtia hatiani daktari huyo ambaye alihamishiwa Ngorongoro kwa ajili ya kazi ili aweze kujibu shutuma ambazo zinamkabili za upotevu wa vifaa na mali za wafadhili kama vile Magari na endapo kama hawatafanya hivyo basi wanannchi wataaambiwa ili waweze kumkamata.

No comments:

Post a Comment