Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Friday 30 May 2014

FRANK LEONARD APATA TUZO YA TANAPA

FRANK LEONARD (KULIA) NA MHARIRI WAKE JOSEPH LUGENDO KWA PAMOJA WAKIWA WAMESHIKILIA MFANO WA HUNDI YA SH MILIONI 1.5 LIYOTOLEWA KWA LEONARD KAMA  MOJA YA ZAWADI KATIKA USHINDI WAKE KATIKA TUZO ZA TANAPA


LEONARD AKIHOJIWA NA MWANDISHI NA MTANGAZAJI WA TBC BENNY MWAIPAJA

LEONARD  AKIWA NA WASHINDI WENGINE WA TUZO ZA TANAPA 2013, KATIKATI NI VEDASTO MSUNGU NA KULIA NI GERALD KITABU WA THE GUARDIAN
MWANDISHI wa magazeeti ya serikali (Dailynews na HabariLeo) mkoani Iringa, Frank Leonard ametwaa tuzo ya uandishi bora wa habari za utalii wa ndani, mwaka 2013.

Leonard ambaye pia ni mmiliki wa mtandao huu wa www.frankleonard.blogspot.com maarufu kama BONGO LEAKS amekuwa mshindi wa pili kwa upande wa magazeti katika tuzo hizo zinazotolewa na Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA).

Kwa ushindi huo amezawadia Sh Milioni 1.5, cheti na ziara katika hifadhi mbalimbali nchini.

Mshindi wa kwanza alikuwa Gelard Kitabu wa The Guardian aliyejinyakulia Sh Milioni 2, ngao, cheti na atapata safari ya kwenda nje ya nchi (moja kati ya nchi za SADC) kutembelea vivutio vya utalii.

Mshindi wa tatu kwa upande wa magazeti alikuwa Jackson Kalindimya kutoka Nipashe ambaye alikabidhiwa hundi ya mfano ya Sh Milioni moja na cheti.

Kwa upande wa redio mshindi wa kwanza katika kipengele hicho cha utalii wa ndani alikuwa David Lwenyagira wa Redio 5 ya Arusha aliyepata Sh Milioni 2, ngao na ziara ya utalii katika moja ya nchi za Sadc.

Mshindi wa pili alikuwa Humphrey Mgonja wa Redio SAUT FM ya Mwanza aliyepata Sh Milioni 1.5, cheti na ziara katika hifadhi mbalimbali hapa nchini; kutoka redioni hakukuwepo na mshindi wa tatu wa habari bora za utalii wa ndani.

Waliobuka washindi wa habari za utalii wa ndani kwa upande wa Televisheni ni Kakuru Msimu wa Star TV aliyekuwa mshindi wa tatu na Kasim Mdame wa Channel Ten aliibuka mshindi wa pili huku nafasi ya kwanza ikikosa mshindi.

Waaliobuka washindi kwa habari za uhifadhi kwa upande wa magazeti ni Salome Kitomri wa Nipashe aaliyeibuka mshindi wa tatu, huku nafasi ya pili na ya kwanza zikikosa washindi.

Kwa upande wa Televisheni, mshindi wa kwanza alikuwa Vedasto Msungu wa ITV, wa pili Raymond Nyamwihura wa Star TV, huku nafasi ya tatu ikikosa mshindi.

Baada ya washindi hao kukabidhiwa zawadi hizo, wakiwa pamoja na wahariri na wanahabari waandamizi wa vyombo mbalimbali vya habari Mei 28 walitembelea hifadhi ya taifa ya kisiwa cha Saanane jijini Mwanza.

BONGO LEAKS

No comments:

Post a Comment