Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Friday 30 May 2014

MAGEREZA NA GEPF WATILIANA MKATABA WA UWEKEZAJI

PIX 1Kamishna Jenerali wa Magereza Jonn Minja (kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (GEPF) Bw. Daud Msangi (kulia) Alhamis 29, 2014
PIX 2Kamishna Jenerali wa Magereza John Minja (kushoto) na Bw. Daud Msangi   Mkurugenzi Mkuu wa GEPF (kulia) wakisaini Mkataba wa Uwekezaji baina ya Taasisi hizo mbili leo Alhamis 29 Mei, 2014 katika Ukumbi wa Mikutano wa Magereza, Jijini Dar es salaam. 

PIX 3Kamishna Jenerali wa Magereza John Minja (kushoto) na Bw. Daud Msangi   Mkurugenzi Mkuu wa GEPF (kulia) wakikabidhiana nyaraka za makubaliano ya uwekezaji baada ya kutiwa sahini.leo Alhamis 29 Mei, 2014 katika Ukumbi wa Mikutano wa Magereza, Jijini Dar es salaam.
Na Deodatus Kazinja-PHQ
 
Jeshi la Magereza nchini kupitia Shirika lake la uzalishaji mali (Prisons Corporation Sole) limetiliana Mkataba wa uwekezaji na Mfuko wa Jamii wa GEPF ambapo majengo ya vitega uchumi yatajengwa katika maeneo ya Kihonda Mkoani Morogoro na Karanga Moshi Mkoani Kilimanjaro.
 
Tukio hilo la utiwaji sahini mkataba  huo limefanyika leo Alhamis 29, 2014 katika ukumbi wa mikutano ulioko Makao Makuu ya Jeshi la Magereza Jijini Dar es salaam. Akiongea katika hafla hiyo Kamishna Jenerali wa Magereza John Minja amesama ni kiu yake kuona mradi huo unaanza kutekelezwa ifikapo Julai Mosi, 2014. Naye Mkurugenzi Mkuu wa GEPF Bw. Daud Msangi amesema ukiwepo ushirikiano wa kutosha miradi hii itaweza kukamilika mapema iwezekanavyo kwa faidi ya pande zote mbili. 

CHANZO FULL SHANGWE

No comments:

Post a Comment