Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Friday 30 May 2014

MILIONI MOJA NA NUSU ZACHANGWA KUNUSURU HOTELI YA CORIDO

tanzania-catholic-churchNA GLADNESS MUSHI, ARUSHA
USHARIKA wa Ngaramtoni mjini  Arusha umechangia zaidi ya shilingi milioni moja na nusu katika harambee ya  kuchangia kulipa deni la Hoteli ya Dayosisi ya Kaskazini Kati,Corrido Spring ya jijini Arusha.
Katika harambee hiyo    iliyofanyika usharikani hapo hivi karibuni Mchungaji  Nodfrey Philipo kutoka Chuo Kikuu Cha Tuamaini Makumira(TUMA)      alisema suala la utoaji ni la mtu na      Mungu wake anayemuamini na ndiyo  maana kila mmoja anapeleka sadaka kule anapo paamini.
Pia alisema kuwa wapo wanaoto a sadaka zao kwa waganga  wakienyeji na wanapokwenda kutambika kwa sababu wanaamini kuwa huko   ndiko mahali sahihi.
Alisema kwa Mkristo safi Kanisani ndipo mahali sahihi pakutoa    sadaka, pia ifahamike kuwa utoaji sio kwa ajili ya mchungaji wala watumishiwengine katika kanisa bali ni kueneza injili  kila mahali”alisema Mchungaji Philipo.
Alifafanua kuwa kila Mkristo anapaswa kutambua kuwa kadri    Mungu anavyoendelea kumbariki na kumtendea mema ndivyo hivyo     yampasa amtolee kwa njia ya sadaka iliaweze kumbariki zaidi.
Alisema lakini mkristo    akiugua na kupata shida ya     kiuchungajaji    ndipo ananza kuona    umuhimu wa   Mchungaji na Kanisa na hata kumjua Mungu ila wakati wa furaha kanisa halinanafasi.
Naye mwinjilisti wa Usharika huo Lamayani Nginuku,alisema kile kidogo ambacho Mungu amekupatia ndicho unachopaswa umtolee kwani uk iwa mtoaji huwezi kuwa masikini.
Pia aliwaasa wakristo kuwa na tabia ya kumshukuru Mungu    kila wakati,pindi wakiwa katika   shida na raha na sio kusubiri wakati wa matatizo ndipo waaze kumtafutaMungu,jambo ambalo halipendezi mbele za Mungu.

CHANZO FULL SHANGWE

No comments:

Post a Comment