Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Wednesday 29 April 2015

BIASHARA YA BINADAMU INATISHA LIBYA

Wahamiaji wakiokolewa baharini
Uchunguzi wa BBC nchini Libya umebainisha mtandao mpana unaotumiwa na walanguzi wanaopata mamillioni ya dolla kupitia usafirishaji wa watu kinyume cha sheria.

Mtu mmoja anaehusika na biashara hiyo amesema kuwa wingi wa watu waliotaka kusafirishwa kwa njia hizo za panya na za hatari umewafanya kuongeza malipo wanayowatoza wahamiaji hao kwa 400%.
Mtu huyo amekiri kuwa boti ndogo wanazotumia ni hafifu lakini hujazwa watu ambao tayari wamewalipa si chini ya dolla 450 kila mmoja, kwa safari hiyo ya kubahatisha ambayo ni dhahiri wengi wao huenda wakapoteza maisha yao.
Mwandishi wetu wa BBC aliyefanya uchunguzi huo anakadiria biashara hiyo kuwa ya thamani ya dolla millioni mia moja na hamsini kila mwaka.
Hivyo ni dhahiri kuwa kundi la wahalifu hao linajitajirisha, na kuwasabishia wengi maafa ya kufa maji na mengineyo , lakini kwa sababu ya ghasia , vita na kuporomoka kwa utawala wa Libya hamna yeyote anaewadhibiti wala kuwawajibisha wahalifu hao.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment