Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Monday 20 April 2015

CHADEMA YAMWAGA SUMU SUMBAWANGA, YASEMA CCM IMEPOTEZA BARAKA ZA MUNGU

Naibu Katibu Mkuu wa Chadema (Zanzibar) Salum Mwalimu akisisitiza jambo wakati akiongea na viongozi wa Vijiji na Mitaa wa chama hicho katika semina ya kuwajengea uwezo iliyofanyika kwenye ukumbi wa Libori mjini Sumbawanga leo hii.

 Viongozi wa Vijiji na Mitaa wa Chadema wakiunga mkono hoja kwenye mkutano huo.
 Silinde yuko makini akisikiliza, hajalala.
 Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mbeya, China wa China.
 Viongozi wa Chadema wakisikiliza maelezo ya viongozi wa vijiji mkoani Rukwa leo hii. 
 Mbunge wa Mbozi Magharibi, David Silinde naye 'akimwaga sumu'.
 Mratibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Frank Mwaisumbe.

Na Mwandishi Wetu, Sumbawanga
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimepoteza baraka za Mungu ndiyo maana mpaka sasa hawajajua nani atakayemrithi Rais Jakaya Kikwete katika uchaguzi wa mwaka huu.
Chadema imesema kwamba, CCM inaandamwa na laana ya damu nyingi za Watanzania zilizomwagika bila hatia, hali ambayo inakifanya chama hicho kishindwe kujua nani atakiwakilisha katika uchaguzi wa mwaka huu, likiwa ni jambo la ajabu kutokea katika historia yake.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya viongozi wa Vitongoji, Vijiji na Mitaa wa chama hicho katika ukumbi wa Libori mjini hapa leo, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema (Zanzibar), Salum Mwalimu, amesema viongozi hao wapaswa kuwa tayari kusimamia haki kwa gharama zozote, kukataa rushwa na kupunguza kero kwa wananchi, na kuonya wasije wakaufanya utawala Chadema kuwa kama wa CCM ambayo inayumba.
“Damu ya Watanzania iliyomwagwa na CCM malipo yake yanalipwa na Mungu… tuna miezi mitatu imesalia tuanze kampeni, lakini mpaka sasa CCM haijamjua mgombea wake, lini imewahi kutokea? Mungu amewachanganya kama wajenzi wa karavati,” alisema Mwalimu.
Alisema viongozi wanaotokana na Chadema wasikubali utawala wao ukakosa baraka za Mungu na njia pekee ni kuwatumikia kwa haki Watanzania.
Mwalimu alionyesha kushangazwa na baadhi ya wafuasi wa Chadema kujiunga na chama cha ACT – Wazalendo kinachoongozwa na Zitto Kabwe na akakiita kuwa ni chama msimu ambacho kitapotea baada ya uchaguzi mkuu ujao.
Alisema Chadema haiwezi kumkataza mtu kujiunga na ACT lakini ni vema wananchi wakaelewa kwamba kile si chama chenye malengo ya kuleta ukombozi kwa Watanzania bali kipo kwa maslahi ya watu wachache na kitadumu kwa muda mfupi tu.
“WanaChadema msikubali kuyumbishwa kwani tumehangaika kuijenga Chadema katika misingi madhubuti ambayo hata wananchi wamekikubali,” alisema.
Awali, Mbunge wa Mbozi Magharibi David Silinde alisema watu walioonyesha nia kugombea nafasi za udiwani na ubunge wasitumie nafasi hiyo kukigawa chama badala yake wawe wepesi kushirikiana na yule atakayeteuliwa ili malengo yao ya kuwakomboa Watanzania katika lindi la umaskini yaweze kufanikiwa.
Mbunge huyo alisema umefika wakati jimbo la Sumbawanga Mjini lipaswa kukombolea kutoka mikononi mwa CCM ili wananchi waondokane na kero zisizo za msingi za kudaiwa michango isiyo na ‘kichwa wala miguu’ ikiwemo ya uandikishaji wa wanafunzi.
“Tangu Chadema ianze kuongoza Halmashauri ya Wilaya ya Momba, michango yote ikiwemo ya uandikishwaji ambayo mzazi alitozwa kati ya Sh20,000 hadi 50,000 imefutwa hali ambayo imeongeza idadi ya watoto wanaoandikishwa darasa la kwanza kutoka 80 kwa darasa moja hadi 300,” alisema.
Naye Mratibu wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini wa chama hicho, Frank Mwaisumbe, alisema Rukwa ndiyo imeoongoza katika mikoa mitano ya Nyanda za Juu Kusini kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, hivyo aliwashukuru wananchi kwa kuiunga mkono Chadema.
“Ninawaomba mfanye hivyo kwenye uchaguzi mkuu ujao ili chama kiweze kutwaa dola na kuwakomboa wananchi kwa kuwatoa katika hali ya ufukara huku watu wachache wakijilimbikizia mali,” alisema.
Mwaishumbe aliongeza kuwa, viongozi waliotokana na Chadema wanapaswa kulipa fadhila hizo kwa kutenda haki kwa wananchi na kuondoa kero ambazo zimekuwa mzigo mkubwa kwao.

No comments:

Post a Comment