Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Wednesday 29 April 2015

BASATA, TCRA WAWATAKA WASANII KUZINGATIA MATUMIZI SAHIHI YA MITANDAO

Displaying 1.jpg
Meneja Mawasiliano wa Mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) Innocent Mungy (Kulia) akiongea na wadau wa Sanaa (hawako pichani) wakati akiwasilisha mada kuhusu matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii kwa wasanii kwenye Jukwaa la Sanaa  lililofanyika Jumanne ya wiki hii makao makuu ya Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Ilala, Sharif Shamba. Kushoto ni Mwanasheria wa BASATA Deogratius Nchimbi.

Displaying 2.jpg
Mwanasheria wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Deogratius Nchimbi (Kushoto) akiongea jambo na wadau wa Sanaa (hawako pichani) mapema wiki hii wakati akihitimisha mjadala kuhusu matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii kwa wasanii uliowasilishwa na Meneja Mawasiliano wa mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kupitia programu ya Jukwaa la Sanaa ya Baraza hilo kwenye Ukumbi wa BASATA ulioko Ilala, Sharif Shamba jijini Dar es Salaam.
Displaying 3.jpg
Mmoja wa wadau wa Jukwaa la Sanaa akiuliza swali kwa Meneja mawasiliano wa TCRA juu ya athari za sheria mpya ya mitandao ya kijamii kwa wasanii na waandishi wa habari.
Displaying 4.jpg
Displaying 5.jpg
Sehemu ya wadau wa Sanaa waliohudhuria programu ya Jukwaa la Sanaa ya Baraza la Sanaa la Taifa mapema wiki hii. 

Na Mwandishi Wetu
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) na mamlaka ya mawasiliano nchini (TCRA) mapema wiki hii wamelaani matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii miongoni mwa wasanii wakati wa programu ya Jukwaa la Sanaa iliyofanyika makao makuu ya Baraza hilo yaliyoko Ilala Sharif Shamba jijini Dar es Salaam.
Akiongea wakati akiwasilisha mada iliyohusu ‘Matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii kwa wasanii’, Meneja mawasiliano wa TCRA Innocent Mungy alisema kuwa wasanii ni kioo cha jamii hivyo kwa namna yoyote ile hawapaswi kuwa sehemu ya uharibifu wa jamii inayowazunguka au kuharibu wajihi (taswira) yao kwa jamii yao.
“Unapokuwa kioo cha jamii, unategemewa kuishi kwa kuwa mfano katika jamii yako. Vijana wengi wanaiga kutoka kwa wasanii ambao ni maarufu. Tunatarajia wasanii wawe mfano kwao” alisisitiza Mungi.
Aliongeza kwamba, msanii anapotumia mitandao ya kijamii kwa kuweka picha chafu, zisizo na maadili au kitu chochote kisicho na staha ni kuchafua wajihi wake mbele ya jamii na hili linampotezea fursa nyingi za kibiashara na kiuchumi maana hakuna kampuni au asasi itakayopenda kufanya kazi na msanii mwenye sifa mbovu.
“Wasanii wanapotumia hovyo mitandao ya kijamii wanachafua wajihi wao katika jamii. Wanajikosesha fursa za kimapato. Mfano; mfanyabiashara anapotaka kutangaza shule yake ya watoto wa awali hawezi kutumia msanii mwenye wajihi mchafu na unaoharibu watoto” aliongeza Mungy.
Alizidi kueleza kwamba wasanii hawana budi kutumia mitandao hii ya kijamii hususan facebook, twitter, instargram, u-tube na kadhalika katika kujitangaza na kuuza kazi zao na zaidi kutenga muda mwingi kutumikia jamii. 
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Idara ya Ukuzaji Sanaa na Masoko wa BASATA, Vivian Shalua alisema kwamba Baraza hilo muda wote limekuwa likisisitiza maadili mema miongoni mwa wasanii maana vijana wengi huwaangalia kama mfano katika maisha yao.
“Kila mara BASATA limekuwa likisisitiza maadili kwa wasanii wote. Kazi hii ni ngumu na inataka wadau wote kushiriki katika kunyoosha maadili ya wasanii na vijana kwa ujumla” alimalizia Shalua.

No comments:

Post a Comment