Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Monday 4 August 2014

MAHASIMU WA SUDAN KUSINI WAKUTANA TENA

Kuna hofu na tisho la njaa Sudan Kusini
Mazungumzo ya amani kati ya serikali ya Sudan Kusini na waasi yameanza tena katika nchi jirani ya Ethiopia.
Mazungumzo hayo, yalikuwa yameahirishwa kwa wiki kadhaa
Zaidi ya watu milioni moja unusu, wameachwa bila makazi kutokana na vita hivyo.Vita vimeendelea nchini Sudan Kusini licha ya makubaliano ya kusitisha vita kufikiwa kati ya pande husika.
Umoja wa Mataifa na mataifa mengine ya Magharibi yameonya kua Sudan Kusini inakabiliwa na tisho la kukumbwa na njaa.
Maafisa wa baraza la usalama la Umoja huo, wanatarajiwa kuzuru nchi hio wiki ijayo.
Katika mazungumzo hayo, serikali na waasi wanatarajiwa kuzungumzia swala la kubuni serikali ya mpito pamoja na muundo wake

Makataa ya makubaliano hayo ni chini ya wiki moja na huenda muda huo usifikiwe.
CREDIT: BBC/SWAHILI

No comments:

Post a Comment