Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Wednesday 20 August 2014

ZIARA YA ACT KATIKA MIKOA 15 TANZANIA


ALLIANCE FOR CHANGE AND TRANSPARENCY (ACT – TANZANIA)
PRESS RELEASE,TAREHE 19 AGOST 2014

Ndugu waandishi wa habari, awali ya yote napenda kuwashukuru kwa majukumu yenu ya kila siku ya kuuhabarisha umma wa watanzania juu ya mambo mbali mbali yanayoendelea ndani na nje ya nchi yetu.
Ninyi ni wadau muhimu katika suala zima la upashanaji habari na mmekuwa mkitekeleza majukumu yenu pasipo upendeleo wala kuhofu jambo lolote, zaidi ya kuongozwa na maadili yanayowaongoza kwa hili sisi ACT-Tanzania tunawapongeza sana.
Ndugu zangu wanahabari kama mnavyojua,ACT-Tanzania ni chama kinachojipambanua katika misingi ya ukweli, uwazi uadilifu na uzalendo kwa ajili ya Taifa letu adhimu la Tanzania na kwa misingi hiyo ndiyo maana leo tumewaiteni kuwajulisha kile tunachorajia kufanya katika ujenzi wa chama hiki kwa ajili ya kuwafikia watanzania wengi zaidi.
Ndugu wanahabari kuanzia kesho mwenyezi mungu akitujaalia uzima chama Cha ACT-Tanzania kitaanza ziara kwa ajili ya kueneza na kukijenga chama hadi katika ngazi za chini, katika azma hii tutafika katika majimbo 65 kwenye mikoa 15 ya Tanzania bara na ziara yote itatumia siku 27.
Ndugu wanahabari katika ziara hii kutakuwa na makundi matatu yatakayogawanya katika mikoa 15 ambapo kundi la kwanza litaongozwa na mwenyekiti wa muda wa ACT-Tanzania Lukas Kadawi Limbu akisaidiwa na mjumbe wa Halmashauri kuu Athuman Balozi na litatumia siku 17 kufika katika majimbo 22 kwenye mikoa mitano
Mikoa hiyo ni Shinyanga Geita,Mwanza Mara na Simiyu na huko watafanya mikutano ya ndani na baadhi ya maeneo watafanya mikutano ya hadhara.
Kundi la Pili litaongozwa na Makamu mwenyekiti akisaidiwa na Naibu katibu mkuu Taifa na litafika katika mikoa ya Tanga,Pwani,Lindi na Mtwara na huko watafanya mikutano ya ndani na ya hadhara kwa baadhi ya maeneo ambayo hayajazuiliwa kwa mikutano ya hadhara kundi hili litatembelea majimbo 15.
Ndugu wana habari kundi la tatu litaongozwa na Katibu Mkuu Samson Mwigamba atakayeambatana na Katibu wa mawasiliano na uenezi, kundi hili litafika katika mikoa sita yenye jumla ya majimbo 28 na litatumia siku 27
Mikoa hiyo ni Singida,Kagera,Kigoma,Rukwa,Katavi na Tabora huko napo kutafanyika mikutano ya ndani na ya hadhara kwa baadhi ya maeneo.
Ndugu wanahabari tunafanya ziara hizi kwa lengo la kukifikisha chama chini zaidi kwa wananchi kama mpango mkakati wetu katika shughuli zinazopaswa kufanywa kabla ya uzinduzi rasmi wa Chama,kwa hivi sasa Chama kipo katika ngazi ya mkoa na kwa upande wa Tanzania bara tuna uongozi wa muda katika mikoa yote isipokuwa katika mikoa ya Rukwa na Njombe na katika mikoa hiyo miwili tayari kuna wanachama waliojiorodhesha kwa ajili ya kuunda uongozi wa mikoa hiyo,hivyo katika ziara hii viongozi wa kitaifa watakapofika Rukwa wataacha uongozi wa mkoa na majimbo huku taratibu za kuupata uongozi wa mkoa wa Njombe zikiwa zinaendelea
Ndugu wanahabari katika ziara hii tutahakikisha kila mahali tutakapopita tunawafunza wanachama na viongozi misingi na imani ya ACT Tanzania kwa ajili ya taifa la leo kesho na keshokutwa.
Mwisho kabisa ACT-Tanzania tunawashukuru wanahabari kwa kutenga muda wenu na kufika kusikiliza kile tulichowaitia,tunawatakia uwajibikaji mwema kwa ajili ya Tanzania iliyo bora
Imetolewa leo na
Idara ya Mawasiliano na Uenezi
0687499466.

No comments:

Post a Comment