Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Sunday 18 October 2015

MAUAJI YA WALAJI NG'OMBE INDIA YAIBUA HASIRA


Mkuu wa chama tawala cha India, cha BJP Amit Shah, amewalaumu wanasiasa wanne wa chama hicho kwa kutoa matamshi ya kutatanisha kuhusu ng'ombe na nyama ya mnyama huyo.
Mmoja alitaka hukumu ya kifo, kwa watu wanaochinja ng'ombe; na mwengine alitoa maanani kisa ambapo Muislamu, aliyetuhumiwa kula nyama ya ng'ombe, alichapwa mikwaju na kundi la watu.
Alidunisha tukio hilo akisema kuwa hiyo ilikuwa ni ajali tu.
Katika kipindi cha mwezi juma lilopita, vifo vingine viwili vya Waislamu, vilihusishwa na ghasia za wazalendo wa Kihindu, kuhusu ng'ombe na ulaji wa nyama ya ng'ombe.
Mapema leo dereva mmoja katika jimbo la Kashmir aliaga dunia kufuatia majeraha aliyopata gari lake lilipowashwa moto
Image copyrightAP
Image captionMauaji ya walaji ng'ombe India yaibua hasira
Wahindu ndio wengi zaidi katika taifa hilo lenye idadi kubwa ya watu wanaoamini na kuabudu mnyama Ng'ombe.
Kinaya ni kuwa wengi wao pamoja na waislamu na wakristu walio wachache hula nyama ya ng'ombe.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment