Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Monday 22 December 2014

LIVERPOOL YALAZIMISHA SARE NA ARSENAL


Liverpool, wakiwa uwanja wa nyumbani Anfield, wamenusurika kupata kichapo toka kwa Arsenal kwa kupata sare ya goli 2-2.

Mshambuliaji Philippe Coutinho alianza kuiandika Liverpool goli la kwanza, kabla ya Mathieu Debuchy hajaisawazishia Arsenal, Olivier Giroud akaongeza bao la pili dakika ya 64.
Beki Martin Skrtel alifunga bao la kusawazisha dakika za nyongeza za kipindi cha pili(90+7) kwa mpira wa kichwa uliomshinda kipa wa Wojciech Szczesny
Mshambulaiji Fabio Borini alitolewa nje baada ya kupewa kadi mbili za njano na kuwafanya liverpool kucheza pungufu.
Katika mchezo mwingine wa Sundeland walipata ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Newcastle United.
Winga Adam Johnson ameibuka shujaa kwa kufunga goli pekee la ushindi kwa upande wa Sunderland, bao la dakika ya 90.
Katika mchezo huo beki wa Newcastle Steven Taylor alipata majeraha baada ya kupasuka eneo la jicho katika heka heka za kumzuia mshambuliaji Steven Fletcher.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment