Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Thursday 25 December 2014

ARSENE WENGER AMWINDA BEKI SERGIO RAMOS WA REAL MADRID

Sergio Ramos, beki wa Real Madrid anayewindwa na Arsene Wenger
Meneja wa Arsenal Arsene Wenger amewasiliana na ajenti wa beki wa Real Madrid Sergio Ramos kuhusu uwezekano wa mchezaji huyo kujiunga na kilabu hiyo ya uwanja wa Emirates.

Ramos mwenye umri wa miaka 28 amekuwa na kilabu hiyo ya Los Blancos kwa takriban muongo mmoja baada ya kuwasili kutoka sevilla kwa kitita cha pauni millioni 20 mwaka 2005.
Hatahivyo ripoti za hivi majuzi zimedai kwamba Ramos huenda akaondoka katika kilabu hiyo ya Santiago Bernabeu baada ya mazungumzo ya kandarasi yake mpya kugonga mwamba.
Na kulingana na mwandishi Esteban Manolete wa AS ,mkufunzi huyo wa The Gunners amewasiliana na wawakilishi wa Ramos ili kuona iwapo anaweza kumvuta mchezaji huyo katika eneo la London kazkazini.
''Wenger amewasiliana na Rene Ramos ajenti na ndugu ya Sergio Ramos'',mwandishi huyo alikimbia kipindi cha La Goleada.
Wenger juma hili alikiri kwamba safu ya ulinzi ya Arsenal haina uongozi baada ya kufungwa bao la dakika za mwisho na liverpool na hivyobasi kupata sare ya 2-2.
CREDIT: BBC/MICHEZO

No comments:

Post a Comment