Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Friday 19 December 2014

WATOTO 8 WAUAWA KATIKA NYUMBA MOJA AUSTRALIA


Polisi nchini Australia wanasema kuwa watoto wanane wamepatikana wakiwa wamekufa kwenye nyumba moja katika mji wa Cairns eneo la Queensland kaskazini ya Australia.

Vyombo vya habari vinasema kuwa watoto hao wote kati ya miezi 18 na miaka 15 walikuwa wamedungwa visu.
Wakazi wa eneo hilo walikusanyika kwa butwaa nje ya nyumba ambako mauaji yalifanyika
Polisi wa eneo la Queensland wanasema kuwa waliitwa kwenda kwa nyumba hiyo baada ya ripoti kutolewa kwamba mwanamke alikuwa amejeruhiwa vibaya. Lakini ndani ya nyumba hiyo polisi waligundua maiti za watoto wanane.
Inaaminika kuwa watoto hao walidungwa kisu hadi wakafa. Polisi wanasema kuwa mtoto mdogo zaidi kati ya watoto hao alikuwa na umri wa miezi 18 na mkubwa zaidi alikuwa na miaka 15.
Mwanamume ambaye anakisiwa kuwa na amri wa miaka 30 amepelekwa hospitalini akiwa na majeraha ya kisu. Ndugu mmoja wa familia hiyo aliwaambia polisi kuwa mwanamke hiyo alikuwa mama wa watoto hao
Polisi hawajamtaja mshukiwa yeyote
Polisi wanasema kuwa hajakamatwa lakini anawasaidia na uchunguzi. Waziri mkuu wa australia Tony Abbott amekitaja kisa hicho kuwa uhalifu mbaya na pia kuzitaja habari hizo kuwa za kuvunja moyo.
Polisi hawajaweza kuthibitisha ambavyo watoto hao waliuawa hadi pale uchunguzi utakapofanyika.
Wanazungumza na watu kadhaa akiwemo mwanamume aliyeonekana karibu na nyumba hio asubuhi na mapema, ingawa hakuna mtu yeyote amekamatwa.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment