Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Monday 19 January 2015

SERIKALI YAPOKEA MSAADA WA VIFAA VYA MICHEZO KUTOKA KWA SERIKALI YA CHINA

Displaying PIX5.jpg
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara (MB)  akibadilishana hati ya makabidhiano ya vifaa vya michezo na Balozi wa China hapa nchini Lu Youqing (kulia) wakati wa hafla ya kukabibidhiana vifaa hivyo mwishoni mwa wiki jijini  Dar es Salaam. (Picha zote na Frank Shija)
Displaying PIX1.jpg
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara (MB) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa hafla ya kukabibidhiwa msaada wa vifaa vya michezo kutoka Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China leo jijini Dar es Salaam.Kutoka kushoto ni Balozi wa China hapo nchini Lu Youqing na Mwakilishi Mkuu wa Wafanyabiashara kutoka China waishio nchini  Lin Zhiyong. Jumla ya vifaa kumi na nne vimetolewa ambavyo ni Roboti ya kujifunzia mpira wa Meza, Kifaa cha kupimia upepo kwa ajili ya Riadha,Nyavu ya mpira wa Meza, Mashine ya kupimia Uzito,Ulingo wa Ngumi, Kompyuta, Printa, Radio Call, mashine ya kutafsiri na kuhesabu matokeo katika riadha na nyaya za umeme vyenye thamani zaidi ya 200.
Displaying PIX3a.jpg
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara (MB)  akicheza Mpira wa Meza na Balozi wa China hapa nchini Lu Youqing (kulia) wakati wa hafla ya kukabibidhiwa msaada wa vifaa vya michezo kutoka Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China mwishoni mwa wiki  jijini Dar es Salaam.
Displaying PIX3b.jpg
Balozi wa China hapa nchini Lu Youqing akielezea namna mmtambo wa Radio Call unavyofanya kazi, katika mwenye blauzi ya kitenge Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara, na Mkurugenzi Msaidizi wa Maendeleo ya Michezo Bibi. Juliana Yassoda
Displaying PIX3c.jpg
Ulingo wa kisasa uliokabidhiwa kwa Serikali ya Tanzania kutoka Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China mwishoni mwa wiki  jini Dar es Salaam.
Displaying PIX4.jpg

Na Benjamin Sawe, WHVUM
Serikali kupitia Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo imepokea msaada wa vifaa mbalimbali vya mchezo wa ngumi na riadha kutoka kwa Serikali ya Watu wa China vyenye jumla ya thamani ya  zaidi ya shilingi milioni 200.
Akizungumza katika makabidhiano hayo Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni  na Michezo Dk. Fennela Mukangara alisema msaada huo ni sehemu ya kuboresha tasnia ya michezo ikiwa ni pamoja na kuendeleza ushirikiano wa muda mrefu baina ya nchi hizo mbili.
“Msaada huu ni kiashirio tosha kwa wananchi wa nchi zote mbili na umekuwepo ukiendelea kuimarika na tunazo fursa za kuendeleza ushirikiano huu kwa manufaa ya wananchi wetu”.Alisema Mheshimiwa Mukangara.
Aidha alimuhakikishia Mheshimiwa Balozi wa China kuwa Watanzania wanathamini mchango mkubwa wenye lengo la kuendeleza michezo hapa nchini kwani China na Tanzania zina historia ya pamoja ya takribani ya miaka 50 mpaka sasa.
Alisema kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa imewasilisha kwenye ofisi ya Ubalozi  wa China mapendekezo ya kuendeleza ushirikiano kupitia sekta ya michezo ambapo matumaini yake ni kuwa kwa kupitia maeneo hayo zitapatikana fursa zaidi kwa vijana kuendeleza ushirikiano baina  ya  nchi mbili kupitia michezo ikiwa ni pamoja na kujifinza mambo muhimu katika tasnia ya Michezo.
Akizungumza  katika  makabidhiano hayo  Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China Mh. Lu Youqing alisema Serikali yake itaendelea kuwa na ushirikiano na Serikali ya Tanzania katika sekta mbalimbali ikiwa ni ishara ya kudumisha ushirikiano baina ya nchi hizo mbili.
Vifaa vilivyotolewa ni pamoja na “Table Tennis 2”, Wind Speed Gage Device 2, “UPS 1, Table Tennis Net” 7, “Electronic Weigher 2”, Computer 1, “Table Tennis Balls”, “Boxing Ring 2”, “Table Tennis 5”, “Printer 1”, “Electronic Cable 6”, “Radio Call 2”, “Anemograph 2”, na Electric Timing and Scoring Interpretation Device For Finishing line 1” ambapo jumla yake ni zaidi ya shilingi milioni 200.

Mpaka sasa  Serikali ya China imeshaipatia msaada Serikali ya Tanzania  jumla ya shilingi bilioni moja ili kuendeleza  sekta mbalimbali nchini.

No comments:

Post a Comment