Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Saturday 29 March 2014

WANAWAKE ELFU SABINI WAKUTANA KULIOMBEA TAIFA


Na Mwandishi wa brotherdanny5.blogspot, Arusha

ZAIDI ya wanawake elfu sabini kutoka maeneo mbalimbali hapa nchini wamekusanyika katika viwanja vya Stadium Jijini Arusha huku lengo halisi likiwa ni kuombea mahitaji yao mbalimbali pamoja na mahitaji ya Taifa la Tanzania.
Aidha wanawake hao waliweza kukutanishwa mapema jana na kituo cha Radio cha Safina katika kongamano la wanawake na mabinti kwa makusudio ya kuwabadilisha mitizamo yao mbalimbali.
Akizungumza na maelfu ya wanawake hao Meneja wa kituo hicho Jovin Abel Msuya alisema kuwa kuna umuhimu mkubwa sana wa kuwasaidia wanawake ili waweze kufika katika malengo yao mbalimbali ambayo wamejiwekea.
Jovin alidai kuwa wanawake wakipewa nafasi nzuri ya kumjua Mungu katika maisha yao basi wataweza kubadilika kwa kiwango kikubwa sana na hata taifa nalo litaweza nalo kubadilika na kisha kupiga hatua
Alifafanua kwa kudai kuwa asilimia kubwa ya familia za sasa zinaharibikiwa sana kwa kuwa wengi wa wanafamilia hasa wanawake wanakosa hofu ya mungu hali ambayo wakati mwingine inasababisha hata taifa kupata wakati mgumu sana.
Amedai kuwa kutokana na hali hiyo sasa kuna umuhimu wa taifa kuwakutanisha wanawake kwa pamoja na waweze kupiga hatua kwani hali hiyo itaweza kusadia sana taifa la Tanzania katika mikakati yake mbalimbali.
"Mwanamke akisimama vema kuanzia kwenye ndoa yake basi hata nchi nayo itakuwa kwenye wakati mzuri na hivyo kila kusudi litaweza kufanikiwa na hapo matatizo mbalimbali ambayo yapo yataisha kabisa kwaiyo ni lazima hata wanawake nao wajue kuwa wana nafasi kubwa sana ya kutetea nafasi yao walionayo kwenye jamii"aliongeza Jovin
Mbali na hayo alidai kuwa kwa sasa nao wanawake wanatakiwa kuinuka katika nafasi zao na kuachana na tabia ambazo wakati mwingine huzaa matunda mabaya kwenye familia zao na hata nchi kwa ujumla ikiwa ni pamoja na kuachana na tabia ya kuamini nafasi za nguvu za giza ambazo wakati mwingine husababisha mafaa makubwa zaidi.
Kwa upande wa wanawake ambao wamehudhuria katika kongamano hilo ambalo liliwahusisha wanawake na mabinti walidai kuwa kwa sasa kuna umihimu wa taasisi za dini kuendelea kuitisha makongamano ya wanawake na mabinti ili kuweza kusaidia jamii kupambana na changamoto mbalimbali.
Wanawake hao walidai kuwa katika makongamano hayo huwa wanapata fursa za kujifunza kwa undani juu ya maadili mema katika ndoa zao lakini hata jinsi ya kutii Amri za Mungu pamoja na ile ya serikali kama walivyokutanishwa na kituo cha Radio Safina.

No comments:

Post a Comment