Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Saturday 29 March 2014

UJENZI WA MNARA WA KATIBA DODOMA


Ndugu zangu,
Kwa yanayoendelea mjini Dodoma katika Bunge Maalum la Katiba, hivi kweli tunategemea tutaipata Katiba mpya yenye kuzingatia maslahi ya Watanzania wote?
Ikiwa wawakilishi wetu tuliowaamini na kuwateua wakajidili mustakabali Katiba ambayo haitaleta kero kama tunazozishuhudia wanaendelea kulumbana, wengine wakipiga kelele almradi siku iende na wao waingize posho, hivi tunayo matumaini tena ya mjadala huo kuzaa matunda?
Naungana na Kipanya katika tafakuri hii kwamba mnara wa Katiba unabomolewa hata kabla ya kujengwa. Kila mmoja anajifanya fundi kuliko mwingine, wengine midomo yao haina tohara wanatema matusi ovyo, wengine wamevimbiwa na posho zinazotokana na kodi zetu na wanaona liwalo na liwe tu, wengine wenzangu na miye wamekwenda kule kuchuma fedha, kwani mbali ya 300,000 wanazopewa, bado wanaangalia upepo unaelekea wapi kwenye neema na kuungana nao ili tu wajaze mifuko yao.
Hii ni hatari sana kwa Watanzania wa leo, ambao daima hao hao ndio wamekuwa wakipiga kelele majukwaani mpaka mishipa ya shingo inawatoka kwamba Katiba ya sasa inahitaji kurekebishwa. Sasa wamelishwa nini Yarabi?
Lakini wakumbuke jambo moja tu, wakifanya mchezo, hata makaburi yao yatakuja kuchapwa viboko na watoto na wajukuu zetu.

Ndugu yenu,
Daniel Mbega
Iringa
0715 070109

No comments:

Post a Comment