Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Saturday 29 March 2014

HAWA NDIO VIBARAKA WA KAGAME WANAOMCHAFUA RAIS KIKWETE

Rais Paul Kagame wa Rwanda

Waandishi wa habari watatu nchini, wametajwa kuwa vinara wa utoaji taarifa za kumkashifu rais Jakaya Kikwete kwa serikali ya Rwanda.


Taarifa zinasema waandishi hao wawili wanafanyakazi katika vyombo vya habari binafsi na mwingine yuko Ikulu ya Rais Jakaya Kikwete. 

Tayari waandishi hawa mashuhuri nchini wamefanya ziara katika nchi za Rwanda, Kongo (DRC), Ufaransa, Ubelgiji, Uganda na Uingereza, ambako pamoja na kukutana na raia wa Rwandwa wanaoishi nchini humo, wamekutana pia na "majasusi ya Kagame."

Aidha, waandishi wamekutana na rais Paulo Kagame, Joseph Kanambe Kabila, Yoweri Museveni na rais wa Ufaransa kwa shabaha ya kumsaidia Kagame kuidhoofisha Tanzania.

“Nakuambia hivi kijana wangu. Wanaosaidia na Kagame kumtukana rais Kikwete, wako humuhumu ndani ya nchi. Kundi ni kubwa mno; lakini ndani yake kuna waandishi wa habari watatu wandamizi nchini,” ameeleza kiongozi mmoja serikalini.

Kupatikana kwa taarifa hizi kumekuja mwezi mmoja baada ya mtandao mashuhuri nchini Rwanda, NEWS of Rwanda (NR), kuchokomoa kinachoweza kuitwa, "Maisha binafsi ya Rais Kikwete."

Katika taarifa hiyo, mtandao huo wa Rwanda unadai mke wa Rais (Mama Salma Kikwete), ni ndugu wa Hayati Jevenalis Habyarimana, aliyewahi kuwa rais wa Rwanda; na kwamba Rais Kikwete mwenyewe ni mtu dhaifu katika masuala ya mapenzi. 

Rais Kikwete na Paul Kagame wamekuwa na vita ya maneno kwa muda mrefu sasa; huku Rwanda ikiituhumu Tanzania kutumiwa na mabeberu wasioitakia mema nchi hiyo.

Tayari waandishi hawa mashuhuri nchini wamefanikiwa kupenya mitego ya maofisa usalama wa taifa mkoa wa Mwanza waliokuwa wanafuatilia nyendo zao, wakati walipokutana na watu wa RPF - Chama cha Kagame, nchini Uganda, miezi mitano iliyopita.

Hiki kilikuwa kipindi ambacho rais Kikwete alifanya ziara mkoani Kagera, ambako pamoja na mengine, aliagiza kutekelezwa “operesheni wahamiaji haramu."

Ugomvi wa Kagame na Kikwete kwa kiasi kikubwa unatokana na serikali ya CCM kukisaidia chama cha upinzani cha Democratic Green Party of Rwanda ili kimuondoe madarakani Kagame na RPF yake.

No comments:

Post a Comment