Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Sunday 30 March 2014

WALEMAVU WA VICOBA WATAPELIWA


Na Oliver Motto, Iringa


KAMA inavyofahamika hali ngumu ya maisha sasa inatoa funzo kwa kila wananchi kuona umuhimu wa kutafuta namna ya kuhifadhi fedha, iwe katika taasisi za kifedha, vikundi vya mitaani (upatu) na hata katika vikundi rasmi vya Benki za Wananchi wa Vijijini -VICOBA.
Asilimia kubwa ya wananchi wa mjini na vijijini wamehamasika kujiunga katika vikundi vya aina hiyo, huku baadhi yao wakikopeshana fedha kwa riba nafuu ili kusaidiana katika changamoto mbalimbali za kimaisha, iwe kusomesha watoto au kumudu mahitaji mbalimbali ya maisha.
Mwamko huo wananchi pia unatokana na serikali  kuwahimiza wananchi kujiunga katika vikundi mbalimbali vya akiba na mikopo, ili wananchi waweze kukopesheka kwa fedha kutoka serikalini na hata kutoka katika asasi mbalimbali, baada ya wananchi kutambulika kupitia katika vikundi vyao.
Jambo hilo ni jema na lenye tija katika maisha haya ya sasa ambayo yanahitaji akili ya ziada, na pia nisema mpango huo unahitaji pongezi kwani umelenga moja kwa moja kumkwamua mwananchi kutoka katika hali ya umasikini wa kipato na hivyo kuwa na uchumi wa kuendesha maisha yake naya familia yake pia.
Lakini kuna msema wa waswahili uliosema "Kwenye wengi kuna mengi" Msemo huo unakamilika kutokana na hivi karibuni kuzuka utata katika VICOBA, ambapo wanachama wa vikundi hivyo wamelalamikia kutapeliwa fedha zaidi ya shilingi Milioni 200  na kiongozi mmoja wa ngazi ya Taifa.
Hatua hiyo imewekwa hadharani katika uzinduzi wa Kikundi cha Vicoba cha Nyerere kilichopo katika eneo la Kibwabwa Kata ya Ruaha Manispaa ya Iringa, na kuwa ubadhirifu huo umefanywa kwa kikundi cha wanachama wa Vicoba Wenye Ulemavu Ilala jijini Dar es Salaam.
Wakilalamikia hali hiyo wanachama hao wamesema licha ya kuhimizwa kujiunga katika vikundi ili kupata mikopo ya fedha, kuna baadhi ya viongozi wamekuwa wakitumia fulsa hiyo kujinufaisha hatua ambayo inatishia kuwasambaratisha.
Wamesema kuna kila sababu wanavicoba wote nchini kuungana katika kudai haki zao pindi   wenzao wanapokumbana na changamoto hizo za kifedha ili kuimarisha umoja wao kwa kuwa tabia hiyo inachangia kuwarudisha nyuma wanavicoba.
George Kalenga mwanachama wa kicoba cha Nyerere amesema baada ya kupata taarifa ya dhuruma ya fedha za misaada ya walemavu wamejikuta wakikata tamaa, ambapo amewataka viongozi wote wapenda haki wa serikali kuchukua hatua dhidi ya tabia ya kiongozi huyo.
Fatuma Mkini naye amesema dhuruma kwa kiongozi mkubwa wa aina hiyo ni jambo la aibu mbele ya jamii, na hasa wadhfa alionao kiongozi huyo ambaye haendani na matukio ambayo amekuwa akiyafanya, na hasa kwa hilo la dhuruma kwa watu wenye ulemavu, ambapo ameiomba serikali kulifuatilia suala hilo ili kiongozi huyo arejesxhe fedha hizo kwa wahusika.
Fatuma amesema kulinyamazia suala hilo ni kudumaza uchumi na kukuza pato la wananchi, kwa kuwa wao wamejiunga katika vikundi hivyo kwa lengo la kujikwamua kiuchumi, huku shinikizo kubwa likitoka kwa serikali.
Spedito Sanga amesema viongozi wa aina hiyo wanatakiwa kupigiwa kelele ili tabia hiyo isikike kwa wananchi, kwa kuwa kulinyamazia kimya jambo hilo ni njia ya kulifanya likue na hivyo tatizo hilo kuwakumba wananchi walio wengi.
Tisiana amesema kiongozi huyo wa ngazi ya juu awali alifanya utapeli wa aina hiyo kwa waratibu wa mikoa yote Tanzania, ambapo aliwahadaa waratibu akiwemo nayeye kuchangia fedha ili kuanzisha hisa.
"Ukweli baadhi ya viongozi wa ngazi za juu wanatutesa sana, sasa kama hili linawavunja moyo wanachama, kwani ametia doa hasa ukiangalia kundi ambalo amelifanyia ubadhirifu ni kundi la walemavu, kiongozi mkubwa kabisa anawarubuni wanachama wakaweke pesa kwenye akaunti yake,".
Amesema waratibu kupitia mpango wa uwahamasishaji wa kujiunga na vicoba kwa kundi la  walemavu, lakini kupitia hili dosari hiyo hata wanachama wengine hawana imani na viongozi na hivyo kazi hiyo kuifanya kwa ugumu zaidi tofauti na awali.
Amesema sasa anataka kuwafikisha Mahakamani wote watakaofika mkoani kwake na kuwavuruga wanachama wa vicoba, kwani hali hiyo imelenga kurudisha nyuma uchumi wa wananchi tofauti na malengo ya uanzishwaji wa vikundi hivyo.
"Hili siwezi kulifumbia macho, kwani hii tabia sasa inaota mizizi, kiongozi huyu amekuwa akituvuruga sana, kwani kuna wakati tulipewa fedha shilingi milioni miamoja na mkurugenzi wa IPP Regnand Mengi, fedha hiyo aling'ang'ania iingizwe kwenye akaunti yake, lakini mpaka leo hii hatujui zipo wapi na zinafanya nini, nitaongea hili mpaka dakika ya mwisho," Alisema.
Amesema kundi la walemavu baada ya kupata taarifa ya utapeli huo wameingia woga kujiunga katika vikundi, huku wengi wao wakitangaza kujiondoa katika umoja huo kwa kuhofia adha hiyo.
Tisiana ameitaka serikali kuingilia kati suala hilo ili kurejesha imani kwa wanachama, kwa madai kuwa kulifumbia macho tatizo hili litaondoa imani pia kwa serikali ambayo nayo imekuwa ikiwahimiza wananchi kujiunga na vicoba.
Nyerere VICOBA wamesema baadhi ya viongozi  wao wamekuwa wakitumia mbinu mbalimbali kwa manufaa yao,  kwa kusanya fedha  za misaada ya vikundi kupitia Akaunti zao binafsi, jambo ambalo linawakatisha tamaa na kamwe hawatakubaliana nalo.
Mapema mwaka 2013 baadhi ya wanachama wa  vikundi vitatu vya VICOBA katika Wilaya ya Kilolo mkoni Iringa walilalamikia kutapeliwa zaidi ya shilingi milioni 30, baada ya kuibuka kwa mtu mmoja na kuwachangisha fedha kwa madai kuwa anataka kuwasaidia na kuongeza hisa zao.

No comments:

Post a Comment