Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Sunday 30 March 2014

SERIKALI YATAKIWA KUSAIDIA SHULE ZA PEMBEZONI


Na Mwandishi wa brotherdanny5.blogspot, Arusha

Serikali imeombwa kuendeleza utoaji wa misaada katika shule zilizopo nje ya miji ili kuweza kuinua kiwango cha elimu na ufaulukwa wanafunzi walioko katika maeneo yaliyo nje ya miji.
Ombi hilo limetolewa na Daniel Josiah mwalimu mkuu msaidizi wa shule ya sekondari ya City Boys iliyopo katika kata ya Olasiti jijini Arusha wakati akiongea na gazeti hili mapema leo.
Josiah alisema kuwa serikali iendelee kutoa misaada yake katika shule zote zilizopo nje ya mji wa Arusha kama vile vitabu,vifaa vya kujifunzia ili kuweza kupunguza mzigo kwa wazazi ama walezi pamoja na utengenezaji wa miundombinu ya barabara na nishati ya umeme ili kuwasaidia wanafunzi kujisomea katika mazingira mazuri.
Aidha Josiah alieleza kuwa shule hiyo iko chini ya uongozi wa kanisa katoliki lengo ni kutoa fursa zaidi kwa vijana wa kiume ambao hawakupata nafasi ya kuendelea na masomo yao baada ya kuhitimu elimu ya msingi ikiwa ni pamoja na luwaandaa kitaaluma katika masomo ya sayansi.
Aliendelea kuwa katika kuwaandaa kitaaluma pia wana waandaa wanafunzi katika maendeleo ya sayansi na teknolojia ili waweze kumudu maisha ya baadaye baada ya kumaliza masomo yao,wanawaandaa kinidhamu kuwa raia bora katika jamii zao.
"Wanafunzi walio wengi hawawezi kujishughulisha na kazi za mikono hali inayo wafanya wengi wao wakimaliza masomo wanashindwa kujiajiri hivyo uongozi wa shule hii umeamua kuwafundisha wanafunzi kazi za mikono wawapo shuleni kama vile kilimo ili hata watakapo maliza masomo yao wasikae bure manyumbani wajishughulishe na kazi mbalimbali"alisema Josiah.
Aliwataka wazazi na jamii kwa ujumla kujali elimu na kuhakikisha kuwa watoto wao wanapata elimu bora ikiwa ni pamoja na kufuatilia maendeleo ya watoto wao,ambapo kazi kubwa wanayoifanya walimu ni kuwaandaa vyema wanafunzi katika masomo ili kuwajengea uwezo wa kuelewa nini wanachofundishwa.
Hata hivyo uongozi wa shule hiyo umeandaa mfumo mpya wa Global Getway inayowahusisha watoto hasa wanafunzi kupata udhamini wa masomo kutoka nchi ya British na kuweza kuwasomesha bure ambapo pia wanawasaidia wanafunzi ambao ni yatima kupitia huduma ya mtoto yesu kuwasomesha bure.

No comments:

Post a Comment