Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Monday 31 March 2014

AFC YADAIWA KUPANGA MATOKEO KUTWAA UBINGWA WA MKOA ARUSHA


Na Mwandishi wa brotherdanny5.blogspot, Arusha


Washindi wa pili wa mkoa wa Arusha timu ya Mana FC wamepinga uhalali wa ubingwa wa soka mkoani Arusha walioupata timu ya AFC wakituhumu mchezo mchafu wa upangaji wa matokeo katika mchezo wa mwisho uliozikutanisha timu ya AFC na Laibon ya  Longido.
Katika mchezo huo AFC ilishinda kwa magoli 9-1 na kuizidi Mana FC kwa tofauti ya magoli baada ya AFC kufikisha magoli 16 dhidi ya magoli 9 ya Mana wakati timu hizo zikiwa zimelingana kwa pointi, hivyo AFC kuwa mabingwa kwa kuizidi Mana kwa tofauti ya mabao 4 kwani AFC imefungwa mabao 3 na Mana ilikuwa haijafungwa hata bao moja.
Meneja wa mana FC Abraham Magumira alisema ukiangalia ushindani uliokuwepo katika Ligi ya Mkoa pamoja na uimara wa timu zote zilizoshiriki hatua ya sita bora ya ligi hiyo ni vigumu mno kwa timu kushinda mabao zaidi ya matano kwani katika michezo yote iliyotangulia hakuna timu iliyofungwa zaidi ya magoli matatu.
Magumira aliongeza kuwa kabla ya mchezo huo walishatoa malalamiko kwa uongozi wa chama cha soka mkoani Arusha juu ya tetesi za AFC kupanga matokeo kwani tayari Mana FC walikua wanaongoza kwa pointi 11.
Alisema kuwa AFC walikuwa wanauwezo wa kufikisha pointi hizo ila mana walikuwa wanawazidi AFC kwa tofauti ya magoli 3 zaidi ya kufunga hivyo AFC walitakiwa kuifunga laiboni zaidi ya mabao 4-0 ili waipiku Mana FC.
Aliongeza kuwa hilo lilijitokeza katika mchezo huo wa mwisho kwani hali ya mchezo ilionyesha waziwazi kuwa laibon walikuja kwa ajili ya kufungwa na mwisho wa siku AFC walishinda 9-1.
Akizungumzia juu ya ubora wa timu Magumira alisema Mana FC imekua na matokeo bora kwani imeshinda michezo mitatu na kutoka sare miwili na haijafungwa hata goli moja tofauti na AFC iliyofungwa magoli matatu na kulazimika kupanga matokeo katika mchezo wa mwisho.
“Timu ya Laiboni haikuwa timu dhaifu kiasi hichi hadi kufungwa magoli tisa kwani katika michezo iliyotangulia ilitoka sare mara mbili na hata michezo iliyopoteza ilifungwa kwa tabu," alisema Magumira.
“Sisi ndio mabingwa halali wa hilo kombe na  na AFC ni mabingwa wa kupangwa na hata kombe walilopewa ni kama wametushikia tu na kama wataendelea na tabia hiyo hawatafika mbali katika mashindano ngazi ya kanda na taifa na kama wanabisha subiri tutaona huko mbeleni,” alitamba meneje huyo wa Mana FC.
Alipoulizwa kuhusu shutuma za upangaji huo wa matokeo Katibu wa Chama cha Soka mkoani Arusha (ARFA) Adam Brown alisema hakuna ushahidi wowote juu ya hilo na kama ni idadi kubwa ya magoli waliyopata AFC ni jambo la kawaida kwenye mchezo wa kandanda kwa vile hakuna idadi rasmi ya magoli inayotakiwa timu kufunga ili ionekane imepanga au kutokupanga matokeo. 
“Kuna timu zinaweza kupanga matokeo hata ya ushindi mdogo wa goli moja ila kinachotakiwa ni ushahidi, hatuna ushahidi wa upangaji wa matokeo na ushindi wa AFC ni wa halali kwani magoli yalikuwa hayana utata na mchezo ulikuwa wa kawaida, kama wana ushahidi watuletee tutaufanyia kazi,” alimalizia Adam Brown.

No comments:

Post a Comment