Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Saturday 29 March 2014

TAHA YATANGAZA NEEMA KWA VIJANA KWENYE MASOKO YA KILIMO HAPA NCHINI




Mwandishi wa brotherdanny5.blogspot, Arusha
Chama cha Wakulima wa Maua, Mboga na Matunda Tanzania (TAHA) kimesema kuwa kwa sasa kina mikakati mbalimbali ya kuwasaidia vijana kuwekeza zaidi kwenye kilimo huku lengo likiwa ni kupunguza tatizo la uhaba wa ajira hapa nchini.
Aidha lengo halisi la kufanya hivyo ni kuongeza ajira kwa vijana wa tanzania husani wale wahitimu wa vyuo vikuu ambao wakati mwingine humaliza masomo lakini hawana ajira.
Hayo yameelezwa na mkurugenzi mtendaji wa TAHA Bi Jacqline Mkindi wakati akielezea mikakati ya chama hicho kwa mwaka huu ambapo mikakati hiyo inalenga kuongeza ufanisi wa chama hicho pamoja na sekta zake.
Aliendelea kwa kusema kuwa vijana ndio nguzo kubwa hapa nchini ambayo ina uwezo wa kujijenga na kujiimarisha kwenye maslai ya taifa endapo kama watapewa fursa ya kufanikisha malengo yao.
Mbali na hilo pia alisema kuwa mkakati huo utaweza kuwa na faida kubwa sana kwa vijana hasa wale ambao ni wahitimu wa vyuo vikuu hapa nchini kwani kwa sasa asilimia kubwa ya vijana ambao wanamaliza vyuo vikuu hukosa ajira na hivyo kujikuta wakiwa wamebaki mitaani.
"Vijana wa Tanzania wana uwezo mkubwa sana wa kuweza kufanya mabadiliko kwenye sekta ya kilimo na hivyo sasa tumepanga wahitimu wa vyuo hasa hivi ambavyo wanajifunza masuala ya kilimo waweze kujiajiri wenyewe na wasisubirie ajira kwani uwezo huo sisi kama TAHA tunao kabisa aliongeza,"Jacqline.
Pia alisema ili kuhakikisha kuwa wanawafikia walengwa ambao ni vijana tayari wameshakubalina na vyuo vya Sokoine pamoja na Tengeru ambapo wahitimu wake wataweza kujiunga moja kwa moja na mpango huo ambao unatekelezwa chini ya TAHA.
Aliwataka vijana wote hata wale ambao sio wahitimu wa vyuo vikuu hapa nchini kuhakikisha kuwa wanatumia kilimo kama ajira na pia kushirikiana na TAHA ili kuweza kufanikisha malengo yao mbalimbali.

No comments:

Post a Comment