Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Thursday 27 March 2014

CHINA HAITAWANYONGA WATANZANIA 15


Dar es Salaam. Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa imesema watu 15 waliokamatwa na dawa za kulevya nchini China, hawatanyongwa na badala yake watafungwa maisha nchini humo kutokana na mawasiliano mazuri ya kidiplomasia baina ya Tanzania na China.
Kwa mujibu wa sheria za nchi hiyo mtu yoyote anayekamatwa na dawa za kulevya adhabu yake ni kunyongwa hadi kufa.
Akizungumza jana na waandishi wa habari juu ya mafanikio ya ziara ya Rais wa Jamhuri ya watu wa China nchini mwaka jana, Xi jinping, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, John Haule alisema nchi hizo mbili zina uhusiano wa muda mrefu na wa kidugu katika nyanja za siasa, uchumi, usalama na jamii.
Haule alisema kutokana na uhusiano mzuri kwa nchi hizo mbili kwa kushirikiana mambo mbalimbali, hivyo wafungwa waliohukumiwa kunyongwa hadi kufa hawatanyongwa na badala yake watafungwa maisha.
  “Tunaushirikiano mkubwa sana ndiyo maana Watanzania waliohukumiwa kunyongwa sasa hivi hawatanyongwa tena na badala yake watatumikia kifungo cha maisha gerezani,” alisema.
 Haule alisema mwaka huu nchi hizo mbili zinajivunia kuadhimisha miaka 50 ya uhusiano ya kidiplomasia ambayo imekuwa na mafanikio katika nyanja mbalimbali.
Alisema kupitia ziara ya Rais Xi Jinping alipata fursa ya kutangaza sera mbalimbali na utayari wa kushirikiana katika kukabiliana na changamoto za kimaendeleo zinazotokea duniani kote.
“Ikumbukwe kwamba, moja ya vielelezo vikubwa kabisa vya ushirikiano wa nchi hizi mbili ni Reli ya Tazara (Reli ya Tanzania na Zambia), Kiwanda cha Nguo cha Urafiki na kwa wale wapenzi wa Soka, Uwanja wa Kisasa wa Mpira wenye uwezo wa kuchukua watu 60,000 wakiwa wamekaa,” alisema Haule.
CHANZO: MWANANCHI

No comments:

Post a Comment