Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Sunday 30 March 2014

KINANA AICHAMBUA RASIMU YA WARIOBA


KATIBU Mkuu wa CCM, Kanali Abdulrahman Omar Kinana
Dar es Salaam. Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana ameikosoa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, akidai imeshindwa kuwasilisha kwa usahihi maoni yaliyotolewa na wananchi.
Alisema Tume hiyo iliyokuwa ikiongozwa na Jaji Joseph Warioba iliwasilisha maoni yaliyokuwa yakiunga mkono mlengo wake badala ya maoni halisi yaliyotolewa na Mabaraza ya Katiba.
Madai hayo mapya ya Kinana yamekuja wakati tayari Tume hiyo imevunjwa rasmi na Rais, kwa mujibu wa sheria.
“Kulikuwa na utaratibu wa kupata maoni kutoka kwenye mabaraza na kuna kata zilihojiwa, tume haijatuambia kwa sababu gani hawakuyasema wanayoyataka wao,” alisema Kinana.
Alisena kuwa kulikuwa na mabaraza 171, lakini Tume pia ilishindwa kutoa takwimu za watu wangapi walikuwa wakiunga muundo wa muungano wa serikali mbili au tatu katika mabaraza hayo.
“Majaji walisema masilahi ya nchi yapo kwenye serikali mbili na wakuu wa mikoa hali kadhalika, lakini mbona Tume hawakusema hayo?” alihoji Kinana.
Katibu Mkuu huyo alikuwa akizungumza katika mkutano wa hadhara ulioandaliwa na CCM Mkoa wa Dar es Salaam jana, kumpongeza Rais Jakaya Kikwete kwa hotuba aliyoitoa katika Bunge Maalumu la Katiba hivi karibuni.
Alisema chama chake kinaunga mkono mchakato wa kupata Katiba Mpya, lakini lazima wahakikishe katiba hiyo ni ya wananchi.
Hii ni mara ya pili kwa viongozi wa juu wa chama hicho kukosoa takwimu za Tume, mara ya kwanza Rais Kikwete alitilia shaka takwimu zilizomo katika ripoti ya Tume hiyo wakati akitoa hotuba yake bungeni.
Kinana alisema pamoja na kuhoji weledi wa Tume ya Warioba pia alitetea hoja ya wingi wa wajumbe wa CCM katika Bunge Maalumu la Katiba.
“Kuna watu kila siku wanalia eti wao wapo wachache na sisi tupo wengi, hii ni lugha ya ajabu kweli kweli, usiku na mchana wanakutana kujadiliana na walipoona chama kimoja kimoja hakiwezi wakaanzisha Ukawa.
“Hao wanaosema tunatumia wingi kupinga masilahi ya nchi, sasa ni masilahi gani yasiyowahusisha CCM?” alihoji Kinana huku akishangaliwa na wafuasi wa chama hicho.

No comments:

Post a Comment