Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Thursday 20 March 2014

KINANA AZINDUA KAMPENI ZA CCM JIMBO LA CHALINZE KWA KISHINDO‏

1
  Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Abdulrahman Kinana akimnadi mgombea wa ubunge jimbo la Chalinze Ridhiwan Kikwete wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye viwanja vya Polisi mjini Chalinze leo ambapo amemuelezea Ridhiwani kama kijana aliyelelewa vyema na chama cha Mapinduzi na wananchi wa jimbo la Chalinze wamchague mgombea huyo kwani ataweza kuwawakilisha vyema bungeni na kutatua matatizo ya jimbo hilo kwakuwa yeye ni mwana CCM na ilani inayotekelezwa ni ya CCM, Uchaguzi wa jimbo la Chalinze unatarajiwa kufanyika Aprili 6 mwaka huu.
2 
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi wa jimbo la Chalinze katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Chalinze leo. 3 
Mgombea wa ubunge jimbo la Chalinze Bw. Ridhiwan Kikwete akiwahutubia wananchi wa jimbo la Chalinze wakati alipokuwa akiomba kura.
Mama Salma Kikwete Mke wa Rais na mjumbe wa Halimashauri kuu kutoka mkoa wa Lindi akimsikiliza mmoja wa waliokuwa wagombea wa jimbo la Chalinze katika mchujo ndani ya Chama cha Mapinduzi Ndugu Imani Madega mara baada ya kumuombea kura Rihiwani Kikwete, katikati ni Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh. Meck Sadik 5 
Mmoja wa waliokuwa wagombea wa jimbo la Chalinze katika mchujo ndani ya Chama cha Mapinduzi Imani Madega kulia akizungumza na Ridhiwani Kikwete mara baada ya kumuombea kura.
6 
Mmoja wa waliokuwa wagombea wa jimbo la Chalinze katika mchujo ndani ya Chama cha Mapinduzi Ndugu Imani Madega akimuombea kura Ridhiwani Kikwete. 7 
Msaniki Sam wa Ukweli kushoto akiwa katika picha ya pamoja na mpenzi wa Chama cha Mapinduzi Mustafa Selemani. 8 
Mama Salma Kikwete Mke wa Rais na mjumbe wa Halimashauri kuu kutoka mkoa wa Lindi akiwahutubia wananchi katika mkutano huo. 9 
Mbunge wa Simanjiro Christopher Ole Sendeka akiwahutubia wananchi wa Chalinze wakati wa mkutano huo.
10 
Nape Nnauye Katibu wa Itikadi, Siasa na Uenezi akizungumza na kukaribisha baadhi ya viongozi katika mkutano huo.
11 
Mama Salma Kikwete Mke wa Rais na mjumbe wa Halimashauri kuu kutoka mkoa wa Lindi akimsikiliza mkuuu wa mkoa wa Dar es salaam Said Meck Sadik. 13 
Kundi la muziki la TOT likitumbuiza katika mkutano huo. 14 
Wananchi waliojitokeza katika mkutano huo wakiwa wamebeba Picha za mgombea ubunge wa jimbo hilo kupitia CCM Ridhiwani Kikwete. 15 
Malkia wa muziki wa Taarab kutoka kundi la TOT Khadija Omar Kopa kulia akiongoza kundi hilo wakati lililpokuwa likitumbiza katika mkutano huo leo. 16 
Marafiki mbalimbali wa mgombea ubunge wa jimbo la Chalinze kupitia CCM Ridhiwani Kikwete waliojitokeza katika mkutano huo wakinyanyua juujuu mabango yenye picha za Ridhiwani Kikwete.
18 
Mama Salma Kikwete Mke wa Rais na mjumbe wa Halimashauri kuu kutoka mkoa wa Lindi kulia, Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana katikati na mgombea ubunge wa jimbo la Chalinze kupitia CCM Ridhiwani Kikwete wakiondoka eneo la Mkutano mara baada ya kumalizika. 19 
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana katikati, Nape Nnauye Katibu wa Itikadi, Siasa na Uenezi na Ridhiwani Kikwete wakitembea kwa miguu kuelekea eneo la mkutano uliofanyika viwanja vya Polisi mjini Chalinze leo.
20 
Mama Salma Kikwete Mke wa Rais na mjumbe wa Halimashauri kuu kutoka mkoa wa Lindi kulia akiselebuka pamoja na akina mama wana CCM mara baada ya kuwasili katika mkutano huo.
(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-CHALINZE)

No comments:

Post a Comment