Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Friday, 10 July 2015

ONYESHO LA YOUNG SCIENTISTS TANZANIA KUFANYIKA AGOSTI 5-7 DIAMOND JUBILEE


Kutoka kushoto ni Makamu wa Rais anayeshughulikia Sera na Uhusiano wa BG Tanzania, Mr. John Ulanga, Mkurugenzi Mtendaji wa Young Scientist Tanzania (YST) ambaye piandiye muasisi mwenza, Dk. Gosbert Kamugisha na Naibu Balozi wa Ireland nchini Tanzania, Brian Nolan wakizungumza na wanahabari (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Young Scientists Tanzania (YST) inayo furaha kuwafahamisha wanafunzi, walimu na watu wote kwa ujumla kuwa onesho lilikuwa likisubiriwa kwa hamu la YST 2015 litafanyika kwa siku tatu katika ukumbi wa Diamond Jubilee kuanzia tarehe 5 hadi 7 August 2015. Hili ni onesho na hitimisho la tafiti za sayansi na tekinologia zilifanywa na wanafunzi wa sekondari kwa takribani mwaka mmoja. Kwa mara nyingine tena, wadhamini wakuu wa maonesho haya BG Tanzania na Irish Aid wamewezesha mafanikio haya.
Ni mafankio makubwa kwa YST kuweza kuifikia mikoa yote kwa kipindi cha miaka mine. Maonesho ya YST 2015 yajumisha wanafunzi 240 na walimu 120 kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara na Zanzibar. Kwa siku tatu za maonesho, wanafunzi wataonyesha kazi zao za ugunduzi na utafiti wa kisayansi kama vile kemia, fizikia na hesabu, biologia na ekologia, teknologia na sayansi ya jamii. Ingawa kazi hizi zinajumuisha maeneo mapana ya kisayansi, kazi nyingi zimejikita katika kutafuta ufumbuzi kwa masuala kama afya, kilimo na usalama wa chakula, usalama, mawasiliano na uchukuzi, nishati na mazingira, elimu, mahusiano na matatizo ya kijamii.
Bado tuna changamoto katika kuinua kiwango cha sayansi kwa shule za sekondari hasa ukizingatia uchache wa wanafunzi wanaosoma sayansi na ufaulu usioridhisha. Ingawa ufaulu umeanza kuimarika kidogo miaka ya karibuni tatizo kubwa limebaki kuwa ukosefu wa sayansi kwa vitendo na matumizi ya sayansi katika kuboresha maisha ya watu....sayansi haiwezi kufanywa kwa kutumia chaki na ubao tu. Maonesho ya YST 2015 yanajaribu kuonyesha kuwa kufanya sayansi ni raha inayotakiwa kufanyika kwa vitendo kumaliza matatizo mbalimbali na inaweza kufanyika popote kwa kutumia vifaa vyovyote. Washiriki wa maonesho ya YST 2015 wataonyesha kupitia kazi zao kuwa kuna namna ya Tanzania kuondokana na umasikini.
Kama njia ya kuwashukuru vijana wabunifu, zawadi zitatolewa kwa wanafunzi wenye kazi nzuri za kisayansi. Takribani wanafunzi 60 watazawadiwa zawadi mbalimbali kama pesa saslimu, medali, vikombe, vifaa vya maabara, na matengenezo ya library na vitabu. Wanafunzi 6 watazawadiwa udhamini wa kusoma vyuo vikuu kusoma shahada za sayansi na teknologia na kuendelea kufanya kazi za kisayansi katika maisha yao. Washindi wa jumla wa maonesho ya YST 2015, pamoja na kupewa pesa na udhamini wa masoma ya chuo kikuu, pia watashinda zawadi ya kwenda Ireland na USA mapema 2016 kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya kimataifa.
YST 2015 ni onesho la wanafunzi wenye vipaji katika sayansi. Pia ni ushahidi katika kuimalika kwa ujuzi wa walimu ambao ni walezi wa wanafunzi hao. Haya yote ni matokeo ya mafunzo kwa walimu ambayo yamekuwa yakitolewa na YST kwa miaka mine iliyopita. Wanafunzi wapatao 2,000 kutoka sekondari za Dar es Salaam wamealikwa kutembelea maonesho na kuja kujionea ubunifu wa vijana wenzao. Wananchi wote wanaalikwa kutembelea maonesho tarehe 6 na 7 August 2015.

No comments:

Post a Comment