Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Friday, 10 July 2015

KOMBE LA KAGAME: AFC LEOPARDS YATWAA KOMBE MOJA KWA MOJA 1984

Kikosi cha AFC Leopards kilichotwaa ubingwa mwaka 1984. Picha kwa hisani  ya kenyapage.net.

Na Daniel Mbega wa www.brotherdanny.com
Mashindano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati 1984 yalifanyika mwezi Januari katika miji ya Nairobi na Mombasa nchini Kenya katika miji ya Nairobi na Mombasa kama ambavyo mtandao wa www.brotherdanny.com unavyochambua. 
Jumla ya timu 10 zilishiriki mashindano hayo yaliyogawanywa kwenye makundi mawili sawia.
Hata hivyo, AFC Leopards ya Kenya ilifanikiwa kulitwaa taji hilo moja kwa moja baada ya kushinda katika miaka mitatu mfululizona safari hii ilitwaa ubingwa miguuni mwa mahasimu wao Gor Mahia kwa kuwanyuka mabao 2-1 kwenye fainali.
Kwenye kundi la Mombasa kulikuwa na mabingwa wa Tanzania Bara, Yanga, Small Simba (Zanzibar), Nkana Red Devils (Zambia), Bereck Power Pack (Malawi), na AFC Leopards (Kenya). Katika kundi la Nairobi kulikuwa na KCC (Uganda), El-Hilal-Obeid (Sudan), National Printing Agency (Somalia), Gor Mahia (Kenya) na Rio Tinto (Zimbabwe).
Mashindano hayo yalikuwa magumu kwa Yanga, kwani mabingwa hao wa Tanzania Bara walionekana kuelemewa sana.
Katika mchezo wake wa ufunguzi Januari 21, Yanga ilicheza na Nkana Red Devils na matokeo yalikuwa kufungwa magoli 2-1, Januari 23 Yanga ikajitupa uwanjani kumenyana na Bereck Power Pack na kufungwa bao 1-0, Januari 25 tena Yanga ilipambana na mabingwa watetezi, AFC Leopards ya Kenya na ikafungwa tena bao 1-0 na katika mechi yake yamwisho dhidi ya Small Simba baada ya kuongoza kwa mabao 2-0 hadi dakika ya 65, Yanga ilijikuta ikifungwa mabao mawili ya haraka haraka na hivyo kufanya matokeo kuwa 2-2. Kwa hali hiyo Yanga ikawa imetolewa bila kunusa nusu fainali.
Katika mashindano hayo ya 11, timu mbili za Kenya, AFC Leopards na Gor Mahia zilifanikiwa kucheza fainali na Leopards ikafanikiwa kulitwaa tena kombe hilo.
Hii ilikuwa ni mara ya pili kwa timu hizo kupambana katika mchezo wa fainali ya michuano hiyo. Mara ya kwanza kwa timu hizo kukutana katika fainali ilikuwa mwaka 1980 mjini Blantyre, Malawi ambapo Gor Mahia ilitwaa ubingwa kwa kushinda mabao 3-2.
Hata hivyo, hii ilikuwa mara ya tatu kwa timu za nchi moja kukutana katika fainali za michuano hiyo. Mara ya kwanza ilikuwa mwaka 1975 wakati Simba na Yanga za Tanzania zilipokutana katika mchezo wa fainali huko Zanzibar na Yanga ikafanikiwa kutwaa ubingwa huo kwa mara ya kwanza kwa kuifunga Simba magoli 2-0.
Kwa kuchunguza kwa undani zaidi kumbukumbu za nyuma za mashindano hayo, hii ilikuwa mara ya tano kwa timu za Kenya kukutana katika michuano hiyo na ilikuwa mara ya nne kwa Gor Mahia na Leopards kumenyana kuwania ubingwa huu.
Mbali na kukutana katika fainali, timu hizi mbili za Kenya zenye upinzani wa jadi kama Simba na Yanga za Tanzania, ziliwahi kukutana tena mara mbili.
Mwaka 1982 zilikutana mjini Nairobi katika mchezo wa nusu fainali ambapo hazikufungana, lakini Leopards ilipewa ushindi baada ya Gor Mahia kugomea sheria ya penati tano tano.
Mwaka 1983 huko Zanzibar zilikutana katika kundi B na Leopards ilishinda mabao 2-1. Pia zimepata kukutana katika mechi za kundi B huko Lilongwe, Malawi mwaka 1980 kabla ya kukutana katika mchezo wa fainali na Leopards ilishinda 1-0 (Wakati huo ikiitwa Abaluhya FC).
Mara nyingine tena Gor Mahia na Luo Union (sasa Re-Union) zilikutana katika mashindano hayo mwaka 1977 mjini Tanga, ambako Luo Union iliyokuwa ikitetea ubingwa wake, iliifunga Gor Mahia 4-2 katika mechi ya kundi B.
Mwaka 1984 Leopards ilikuwa na wachezaji wazuri sana kama golikipa Mahmoud Abbas, Mike Weche, Patrick Shilasi, John Arieno, Josephat Murila, Issa Suleiman, Dan Musuku, Ben Musuku, Wilberforce Mulamba, Dakta Joe Masiga, Tonny Lidonde, Mike Amwayi, Haggai Mirakau, Francis Lubembe na Ineah Isabwa.

Kundi A
      Gor Mahia      1-1 Kampala City Council
      Printing Club  1-1 Rio Tinto
      El Hilal       0-3 Gor Mahia
      Kampala CC     1-1 Rio Tinto
      Rio Tinto      1-1 El Hilal 
      Gor Mahia      3-0 Printing Club
      Printing Club  2-3 Kampala City Council
      Gor Mahia      2-0 Rio Tinto
      Printing Club  3-3 El Hilal 
      El Hilal       1-3 Kampala City Council

 1.Gor Mahia          4  3  1  0  9- 1  7  [Kenya]
 2.Kampala CC      4  2  2  0  8- 5  6  [Uganda]
 3.Rio Tinto           4  0  3  1  3- 5  3  [Zimbabwe]
 4.Printing Club   4  0  2  2  6-10  2  [Somalia]
 5.El Hilal              4  0  2  2  5-10  2  [Sudan]

Kundi B
      Yanga             2-1 Nkana Red Devils
      AFC Leopards   1-0 Small Simba
      Berec PP       1-0 Yanga
      Nkana RD       0-0 AFC Leopards
      Small Simba    0-0 Berec Power Pack
      Yanga       0-1 AFC Leopards
      Berec PP       0-2 Nkana Red Devils
      Small Simba    2-2 Yanga
      AFC Leopards   0-1 Berec Power Pack
      Nkana RD       1-1 Small Simba

 1.AFC Leopards      4  2  1  1  2- 1  5  [Kenya]
 2.Berec Power Pk.  4  2  1  1  2- 2  5  [Malawi]
 3.Nkana Red Dev.  4  1  2  1  4- 3  4  [Zambia]
 4.Yanga                    4  1  1  2  4- 5  3  [Tanzania]
 5.Small Simba        4  0  3  1  3- 4  3  [Zanzibar]

Nusu fainali
      AFC Leopards   1-0 Kampala City Council
      Gor Mahia      1-0 Berec Power Pack

Mshindi wa tatu
      Kampala CC     1-0 Berec Power Pack

Fainali
      AFC Leopards   2-1 Gor Mahia

KUMBUKUMBU HIZI ZIMEANDALIWA NA MTANDAO WA www.brotherdanny.com. Ukirejea weka chanzo cha habari tafadhali.


No comments:

Post a Comment