Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Friday 31 July 2015

MARADONA AMTUHUMU MKEWE KUMWIBIA FEDHA

Diego Armando Maradona
Nguli wa soka duniani, Diego Maradona amemtuhumu mke wake wa zamani Claudia Villafañe kwamba kamuibia kiasi cha fedha zipatazo dola milioni tisa, katika akaunti yake ya benki.

Akizungumza katika matangazo ya moja kwa moja ya Luninga,Maradonna amesema Villafañe ambaye alikuwa mpenzi wake wa zamani ni mwizi. Hata hivyo Villafañe amepinga vikali madai na kudai kuwa yeye si mwizi na hakuiba fedha hizo.
Wapenzi hao ambao walikutana katika mji uliokithiri kwa umasikini huko Buenos Aires kabla ya Maradonna kuwa maarufu na kuwa miongoni mwa wachezaji mahiri duniani katika historia ya soka,waliachana kimapenzi kutokana na kutofautiana.
Watoto wao wawili Dalma na Giannina, wamekaririwa kwenye mtandao wa twitter wakimtetea mama yao wazi wazi na kwamba hahusiki na upotevu huo wa fedha za baba yao.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment