Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Monday 27 July 2015

MAN UNITED YAMSAJILI KIPA SERGIO ROMEO

Sergio Romeo
Kipa Sergio Romero, aliyekuwa akiichezea klabu ya Sampdoria, amejiunga na vijana wa Louis Van Gaal baada ya kukamilisha muda wa mkataba wake na Sampdoria.

Romero aliwahi kucheza chini ya Van gaal katika timu ya AZ Alkmaar ya Uholanzi iliyotwaa ubingwa wa kombe la ligi ya Uholanzi mnamo mwaka wa 2009.
Kipa huyo ametia saini mkataba wa miaka mitatu na anatarajiwa kuchukua nafasi ya kipa wa akiba, Victor Valdes ambaye ameambiwa yuko huru kuihama klabu hiyo na Van Gaal.
Romero alikuwa katika timu ya taifa ya Argentina iliyofika fainali ya Copa America mwaka huu na kombe la dunia nchini Brazil mwaka uliopita.
Kwa sasa kipa huyo ameungana na wana-devils katika kambi ya mazoezi ya timu hiyo nchini Marekani.
Mchezaji huyo ni miongoni mwa wachezaji waliofunzwa na Van gaal ambao wameungana naye Old Trafford wengine wakiwa ni Memphis Depay, na Daley Blind.
Hatua ya kumsaini Romero inaonekana ni kama njia ya kupiga jeki idara ya ulinzi katika Manchester United huku Mhispania, David De gea akiendelea kusakwa na ReaL Madrid.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment