Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...
Saturday, 11 July 2015
MEMBE APONGEZWA KUINGIA TANO BORA
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM),
Abdulrahman Kinana akizungumza wakati wa kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM (NEC)
katika ukumbi wa Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma jana. Katikati ni Mwenyekiti
wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete na Makamu Mwenyekiti Visiwani na Rais wa
Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein.
Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete
akizungumza wakati wa kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) katika ukumbi wa
Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma jana. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM
Visiwani na Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein na Katibu Mkuu wa CCM,
Abdulrahman Kinana.
SIASA SIO UADUI.... Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe (kushoto) akipongezwa na Waziri Mkuu
mstaafu Edward Lowassa baada ya kuteuliwa kuingia katika tano bora ya wawania
urais katika uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi ya chama hicho, kabla ya kuanza kwa
kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) katika ukumbi wa Makao Makuu ya CCM
mjini Dodoma jana.
Baadhi ya Wajumbe wa kikao cha Halmashauri Kuu ya
Chama Cha Mapinduzi (CCM) (NEC) wakimpongeza Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe (kulia),
baada ya kuteuliwa kuingia katika tano bora ya wawania urais katika uchaguzi
mkuu ujao kwa tiketi ya chama hicho, kabla ya kuanza kwa kikao cha NEC, katika
ukumbi wa Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma jana.
No comments:
Post a Comment