Kikosi cha Yanga cha mwaka 1994. Waliosimama kutoka kushoto ni Salum Kabunda 'Ninja', Constantine Kimanda, Steven 'Abdulmalik' Casmir Nemes, Kenneth Mkapa, na Selemani Mkati. Waliochuchumaa ni Nico Bambaga 'Machine', Sekilojo Chambua, Edibily Lunyamila, James Tungaraza 'Boli Zozo', na Said Nassoro Mwamba 'Kizota'.
Na Daniel Mbega wa www.brotherdanny.com
HAKUNA michuano
ya KLabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati iliyokuwa na mizengwe na upendeleo wa
wazi kama ya mwaka 1994. CECAFA ilifumbia macho mambo maovu kabisa kwenye
kandanda, ikiwabeba wenyeji kwa mbeleko ya chuma hadi kufanikisha azma yao.
Mtandao wa www.brotherdanny.com unaendelea
kuwaletea uchambuzi wa kihistoria katika mashindano haya wakati tukielekea
kwenye michuano ya mwaka huu ambayo itaanza Jumamosi hii jijini Dar es Salaam.
Kwanza kabisa Silver
Strikers ya Lilongwe, Malawi iliwasili siku chache kabla ya mashindano lakini
ilikataliwa na Katibu Mkuu wa CECAFA James Tirop wa Kenya kwa maelezo kwamba
ilichelewa kujiandikisha;
Gor Mahia ya
Kenya ilichelewa kuwasili katika mechi ya ufunguzi dhidi ya El Merreikh, lakini
haikuadhibiwa;
Kwa hiyo Silver
Strikers ilibakia mjini Khartoum kwa siku chache kwa matumaini ya kuruhusiwa
kushiriki bila mafanikio, hatimaye ikarejea kwao ikiwa imepoteza gharama nyingi.
Kutokana na hali
hiyo ya ubabashaji, Malawi ilijitoa CECAFA, ikifuatia hatua ya awali ya Zambia
na Zimbabwe, na hazikurejea tena, badala yake zikajiunga na Shirikisho la Soka
Kusini mwa Afrika (COSAFA).
Michuano ya mwaka
1994 ilifanyika katika miji ya Khartoum na Port Sudan. Kundi A lililokuwa mjini
Khartoum lilizishirikisha timu za El-Merreikh (Sudan), Simba (Tanzania),
Express (Uganda) na Gor Mahia (Kenya).
Kundi B la mjini
Port Sudan lilikuwa na mabingwa watetezi, Yanga (Tanzania), El-Hilal Port
Sudan, Electric (Ethiopia) na Shangani (Zanzibar).
Michuano hiyo
iliyoanza Januari 8 na kumalizika Januari 20 iliingia dosari Januari 14 wakati
Simba, ikiwa inaongoza kwa mabao 2-1 dhidi ya El-Merreikh, ilizimiwa taa
uwanjani na wachezaji wake kupigwa na mashabiki, ambapo kiungo Nico Kiondo
alichomwa kisu.
Simba, ambayo
ilikuwa inaongoza katika kundi A, iliamua kujitoa mashindanoni na ilikuwa
inazishauri timu nyingine za Tanzania, Yanga na Shangani zijitoe. Hata hivyo,
timu hizo mbili hazikujitoa.
Kwa hali hiyo,
El-Merreikh iliyokuwa inashika nafasi ya pili kwenye kundi hilo, sasa
ilipangiwa kucheza na mshindi wa pili wa kundi B, El-Hilal. Lakini katika hatua
ya kushangaza, El-Hilal iligoma kucheza na El-Merreikh kwa madai kwamba hiyo
haikuwa timu ambayo ilipaswa kupambana nayo na hivyo Shangani iliyoshika nafasi
ya tatu kwenye kundi B ikapambana na El-Merreikh katika nusu fainali, ambapo
ilifungwa bao 1-0.
Yanga nayo
ilibidi ipambane na Express waliokuwa washindi wa tatu kwenye kundi A. Katika
mchezo wa nusu fainali, Yanga ilitolewa na timu hiyo ya Uganda kwa penati 5-4
baada ya kutoka sare ya bao 1-1 hadi muda wa ziada, hivyo ikawa imeutema
ubingwa huo iliouchukua nchini Uganda mwaka 1993. Katika kutafuta mshindi wa
tatu, Yanga iliifunga Shangani mabao 2-1.
El-Merreikh ndiyo
iliyotwaa ubingwa huo kwa kuifunga Express mabao 2-1 kwenye fainali.
Kwa kweli
michuano hiyo ilikuwa na dosari kubwa, kwani tangu awali ilionekana wazi kwamba
Wasudani walikuwa wanapendelewa na wala CECAFA haikuweza kuchukua hatua zozote
za tahadhari hata pale wachezaji wa Simba walipofanyiwa fujo.
Hebu tuangalie
namna mashindano hayo yalivyokwenda:
08/01/1994:- Shangani
0 vs El-Hila 1
09/01/1994:-
Yanga 0 vs Electric 0
09/01/1994:- Simba
1 vs Express 2
09/01/1994:- El-Merreikh
1 vs Gor Mahia 1
11/01/1994:-
Shangani 2 vs Electric 1
11/01/1994:- Express
1 vs El-Merreikh 2
12/01/1994:-
Yanga 1 vs El-Hilal 1 (Fumo Felician/Amir Moussa)
12/01/1994:- Simba
1 vs Gor Mahia 0
14/01/1994:-
*Simba 2 vs El-Merreikh 1 (Ramadhani Lenny, Nteze John/?) - mchezo ulivunjika
dakika ya 88).
14/01/1994:- Yanga
2 vs Shangani 1
14/01/1994:- Express
1 vs Gor Mahia 0
14/01/1994:- El-Hilal
0 vs Electric 0
Kundi A
1.El Merreikh 3
2 1 0 3-
2 5
[Sudan]
2.Express FC 3
2 0 1 4-
3 4
[Uganda]
3.Simba SC 3
1 0 2 3-
2 2
[Tanzania]
4.Gor Mahia 3
0 1 2 1-
4 1
[Kenya]
[NB: bila mabao ambayo El Merreikh iliyopewa
dhidi ya Simba]
Kundi B
1.Young Africans 3
1 2 0 3-
1 4
[Tanzania]
2.El Hilal 3
1 2 0 2-
1 4
[Sudan]
3.Small Simba 3
1 0 2 2-
3 2
[Zanzibar]
4.Mebrat Hail 3
0 2 1 0-
2 2
[Ethiopia] [aka EELPA]
NUSU FAINALI:
17/01/1994:-
El-Merreikh 1 vs Shangani 0 (Zahir Abdulghani 90)
18/01/1994:-
Yanga 1 (4) vs Express 1 (5) (Constantine Kimanda 14, pen: Stephen Mussa,
Kenneth Mkapa, Tungaraza, Mohammed Hussein/ Robert Aloro 52, pen: )
MSHINDI WA TATU:
20/01/1994:-
Yanga 2 vs Shangani 1
FAINALI:
20/01/1994:-
El-Merreikh 2 vs Express 1 (Fattah Rahman Santo (mawili)/Issa Sekatawa).
[kadi nyekundu katika kipindi cha pili: Fatah
El Rahman Faraq (Merreikh) na Abdul Nsubuga (Express)]
KUMBUKUMBU
HIZI ZIMEANDALIWA NA MTANDAO WA www.brotherdanny.com.
Tafadhali ukirejea weka chanzo cha habari.

No comments:
Post a Comment