Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Tuesday, 21 July 2015

LUCAS SELELII,KIGWANGALLA JINO KWA JINO NZEGA VIJIJINI

Lucas Lumambo Selelii akiwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda wakati wa Bunge la Tisa.

Na Hastin Liumba, TaboraMAKADA  wawili  wa CCM wilaya ya Nzega  Lucas  Lumambo Selelii  na Dkt,Hamisi kigwangalla wameonyesha kukabana koo katika kuwania ubunge jimbo la Nzega vijijinni huku sintofahamu  ya nani ataibuka kidedea kuteguwa  kitendawli  hicho.

Dkt,Hamis Kigwangalla alisema shinikizo la kugombea Nzega Vijijini limetoka kwa wananchi wanaotambua umuhimu wake na hivyo walimuomba kugombea eneo hilo.

Alisema endapo chama hicho kitampatia ridhaa  ya kupeperusha bendera na kuchaguliwa kuwa mbunge wa jimbo atahakikisha wananchi wanapata maendeleo na kuongeza kuwa wachimbaji wadogo wa dhahabu hatochoka kuwatetea.

Kigwangalla  alisema katika kipindi cha miaka mitano wananchi wa jimbo la Nzega amewatumikia na kuwapatia maendeleo  katika Nyanja za maji,Afya na Elimu.

Kwaupande wake Lucas  selelii aliyewahi  kuwa mbunge wa  jimbo  la Nzega  kwa kipindi cha miaka 15 alichukua fomu  kimya  kimya    katika ofisi  hizo za chama  wilaya bila kuzungumza na vyombo vya habari.

Hata hivyo  inaelezwa jimbo hilo linatarajia kuwa na upinzani mkali kati  ya makada hao wawili licha ya kuwepo kwa  kada wengine wawili waliojitosa kuchukua fomu za kuwania  kiti hicho katika jimbo hilo Jonh  Dotto  pamoja  na Paul  Kabelele.

Katika  jimbo  la Nzega  mjini  na Hussein  Bashe,Joseph  Ngulumwa mchuano utakuwa mkali kati ya wawili hao.

Mchuano mkali mwingine utakuwa kati ya Emmanuel Mwakasaka jimbo la Tabora mjini, huku jimbo la Urambo Mashariki mke wa spika wa zamani Samweli Sitta, Magreth Sitta watachuana vikali na Mtumishi kampuni ya Tigo Ali Maswanya.

No comments:

Post a Comment