Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Tuesday, 21 July 2015

JAMII YAASWA KUJALI MAKUNDI MAALUMU YENYE UHITAJI

Mkurugenzi wa Kanda ya Ziwa kutoka Tigo Bw. Ally Maswanya akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kufafanua huduma mbalimbali za TIGO.

Na Hastin Liumba,TaboraJAMII imeaswa kuwalea na kuwatunza watoto  yatima   ambao muda wote wamekuwa ni wahitaji wa misaada ili waweze kujimu kimaisha.

Hayo  yamesemwa  na meneja wa Kanda wa  kampuni  ya simu  za mkononi Tigo Ali Maswanya wakati wa chakula maalunmu cha usiku kilichoandaliwa na kampuni ya Tigo mkoani Tabora.

Akizungumza na  baadhi ya wageni na watoto  yatima wa kituo cha Igambilo Center alisema jamii  imewasahau watoto  yatima na kujikuta watoto hao wakiishi maisha ya kuomba omba.

Alisema kuwa watoto yatima wana haki kama watoto wengi hivyo wanapaswa kufarijiwa kwa nyakati mbalimbali ikiwa na kushirikishwa katika shuguli za maendeleo.

Kwa upande wake kaimu Mkuu wa Mkoa Suleiman Kumchaya ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Tabora Mjini alisema makampuni mengine yana paswa kujali makundi maalum kwa nyakati mbalimbali nasi katika vipindi vya kama hivyo.

Kumchaya aliitaka jamii kuilinda amani katika kipindi hiki cha uchaguzi mkuu mwezi Octobar mwaka huu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa kampuni ya Tigo kanda ya ziwa Ally Maswanya alisema kampuni hiyo imeamua kushirikiana na waislam pamoja na watoto yatima katika Futari ilikudumisha upendo na waumini wa Dini hiyo.

Alisema kuwa kampuni hiyo imetoa zawadi ya sikukuu  ya Iddi  kwa watoto  yatima iliwaweze kufurahia sikuu hiyo  kama watoto wengine waishio na wazazi wao.

No comments:

Post a Comment