Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Friday 31 October 2014

WAHUDUMU WA EBOLA WAONGEZEWA MOTISHA

Gavana wa jiji la New York Andrew Cuomo
Serikali ya Marekani imeongeza fedha kwa wafanyakazi wa sekta ya afya wanaowahudumia watu walio athiriwa na virusi vya ugonjwa wa Ebola ,lengo ni kuwavutia manesi na madaktari wengi zaidi kwenda kutoa huduma katika nchi za Afrika Magharibi.

Mpango huo umepata baraka zote za ikulu ya Marekani ,mbali na hayo wataalamu hao wa afya ambao watajitolea utaalamu wao , lakini pia wamehakikishiwa malipo manono,huduma za afya na kuhakikishiwa usalama wa ajira zao, pindi watakapo rejea nchini Marekani baada ya kazi.
Gavana wa mji wa New York Andrew Cuomo amesema changamoto ya ugonjwa wa Ebola inahitaji uwajibikaji wa kina wa dunia yote,ikiwemo kuwatia moyo wafanyakazi wa afya kutoka Marekani ili wakubali kwenda kutoa huduma za afya kwenye nchi zilizoathiriwa na ugonjwa wa Ebola.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment