Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Friday 31 October 2014

MWANDISHI WA AL-JAZEERA AKAMATWA MISRI

Nembo ya Kituo hicho
Mwanafunzi wa chuo kikuu nchini Misri ambaye hufanya kazi ya kupiga picha na uandishi wa runinga wa kituo cha Al- Jazeera amekamatwa na kuwekwa korokoroni.

Mwanafunzi huyo mwenye umri wa miaka 21,ambaye jina lake halikufahamika mara moja ,alikamatwa na askari kanzu wakati akipiga picha wakati wa maandamano katika mji wa Mahalla,ulioko upande wa kaskazini mwa mji mkuu Cairo.
Mwandishi na mpiga picha huyo alikuwa na kijitabu kidogo chenye maandishi na maneno yanayotumiwa jeshini na polisi.waandishi wawili waliokuwa pamoja naye wakiwa na kamera walifanikiwa kukimbia.
Mwezi June mwaka huu nchi hiyo iliwafunga waandishi wawili wa Al-Jazeera miaka saba gerezani na mwingine watatu, alihukumiwa miaka kumi gerezani kwa kosa la kusambaza habari za uongo na kuunga mkono kundi lililopigwa marufuku la Muslim Brotherhood.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment