Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Wednesday 20 November 2013

DK. NCHIMBI AKUTANA NA VIONGOZI WA SHIRIKA LA MISAADA LA HANNS SEIDEL FOUNDATION


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi (kushoto) akizungumza na ujumbe wa Shirika la Misaada la Hanns Seidel Foundation masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya wizara yake na shirika hilo. Wapili kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa shirika hilo, Dk. Peter Witterauf, anayefuata ni Mkuu wa shirika hilo, Kanda ya Afrika, Klaus Liepert, na Mwakilishi Mkazi wa Shirika hilo nchini Tanzania, Konrad Teichert. Viongozi wa Shirika hilo lenye Makao Makuu yake jijini Munich nchini Ujerumani walimtembelea Waziri Nchimbi ofisini kwake, jijini Dar es Salaam leo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi (kushoto) akipokea zawadi kutoka kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Misaada la Hanns Seidel Foundation, Dk. Peter Witterauf. Kulia ni Mkuu wa shirika hilo, Kanda ya Afrika, Klaus Liepert. Viongozi wa Shirika hilo kutoka Makao Makuu, Kanda ya Afrika pamoja na Mwakilishi Mkazi wa shirika hilo nchini walimtembelea Waziri Nchimbi ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya wizara yake na shirika hilo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi (wa pili kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Shirika la Misaada la Hanns Seidel Foundation. Katikati ni Afisa Mtendaji Mkuu wa shirika hilo, Dk. Peter Witterauf, wa pili kulia ni Mkuu wa shirika hilo, Kanda ya Afrika, Klaus Liepert. Kushoto ni Mwakilishi Mkazi wa Shirika hilo nchini, Konrad Teichert na kulia ni Naibu Kamishina wa Polisi Makao Makuu, Tathimini na Ufuatiliaji, (DCP) Omar Rashid. Viongozi wa Shirika hilo lenye Makao Makuu yake jijini Munich nchini Ujerumani walimtembelea Waziri Nchimbi ofisini kwake, jijini Dar es Salaam leo kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya wizara yake na Shirika hilo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani.
KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI

WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

No comments:

Post a Comment