Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Monday, 18 May 2015

SERIKALI YAWAASA VIJANA KUJIEPUSHA NA NGONO ZEMBE

Displaying namt 1.jpg
Mkuu wa Kitengo cha Sheria Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Ester Riwa akiongea na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo Bw. Martin Mtani wakati wa ziara ya mafunzo ya ujasiriamali na jinsi ya kujikomboa kiuchumi kwa Vijana wa Halmashauri hiyo mkoani Ruvuma.wa kwanza kushoto ni Afisa Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Amina Sanga.(Picha na Benjamin Sawe-WHVUM).

Displaying namtu 2.jpg
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo Bw. Martin Mtani akisisitiza jambo kwa timu ya wataalam kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wakati wa ziara ya mafunzo kwa vijana wa Wilaya hiyo yenye lengo la kuwakwamua kiuchumi.(Picha na Benjamin Sawe-WVUM)
Displaying Namtu 3.jpg
Mkuu wa Kitengo cha Sheria Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Ester Riwa akiongea na Vijana wa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo juu ya umuhimu wao wa kujishughulisha na ujasiriamali ili kukuza uchumi wa taifa na kujikomboa kiuchumi.(Picha na Benjamin Sawe- WHVUM)
Displaying NAMTU 4.jpg
Afisa Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Amina Sanga akitoa mada ya jinsi ya mfuko wa Vijana unavyoweza kuwasaidia vijana wa Halmashauri ya Namtumbo Mkoani Ruvuma wanaokidhi vigezo vya ujasiliamali ili kujiinua Kiuchumi.
Displaying namt 5.jpg
Afisa Ushirika wa Halmashauri ya Namtumbo akitoa mada kwavijana wa Halmashauri hiyo juu ya uanzishwaji wa Saccos ikiwa ni juhudi za Serikali kuwainua vijana kiuchumi.(Picha na Benjamin Sawe- WHVUM).

Na Benjamin Sawe, Namtumbo-WHVUM
Serikali imewaasa vijana kujiepusha na ngono zembe ikiwa ni pamoja nakujiepusha na matumizi ya dawaza kulevya ili waweze kujiletea maendeleo yao na kujiinua kiuchumi.
Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Kitengo cha Sheria Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wakati wa mafunzo elekezi ya jinsi ya kujikwamua kiuchumi kwa vijana wa halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo.
Alisema  vijana kujihusisha na ngono zembe na matumizi ya dawa za kulevya kutawafanya kuwa dhaifu na kushindwa kuchangia katika ujenzi wa taifa na kujiinua kiuchumi.
“Nawashauri msijihusishe na ngono zembe na matumizi ya dawa za kulevya kwani mikopo mtakayoipata mtashindwa kuirejesha kwa wakati hivyo mtaisababishia serikali hasara kubwa”.Alisema.
Bibi.Riwa amesema kuwa jitihada za awali zifanywe na vijana wenyewe kwakuwa  na mwamko wakuleta maendeleo yatakayotokana na miradi endelevu na yenye malengo kwani kwakufanya hivyo wataweza kukabiliana na hali ya maisha ya duni na kuwa mfano katika jamii na taifa kwa ujumla.
Aidha Afisa Maendeleo ya Vijana Wilaya ya Namtumbo Bi.Rahiya Nasser.amewataka vijana wa Namtumbo   kutokupenda kubebwa kwakupewa fedha za bure kwakununuliwa na wanasiasa bali wazidi kujijengea mazoea ya kuwekeza na kuchukua mikopo inayotolewa na Serikali kwa vijana yenyeribana fuu na kurejesha fedha hizo kwa wakati ili vijana wengine waweze kufikiwa na fursa hiyo.
Akizungumza na vijana wakati wa semina hiyoAfisaUshirika Halmashauri yaWilaya ya hiyo Bw. Theophily Ngonyani amewataka vijana kutokuwa watu wakusukumwa kutafuta maendeleo yao bali wawajibike nakutafuta fursa zilizopo ili kuweza kuondokana na hali duni ya maisha.
“Vijana wenzangu hamjazaliwa kuishia hapo mlipo, msipende kusukumwa nawatu kutafuta maendeleo yenu ,changamkieni fursa zilizopo nakuwajibika katika jamii zenu bila ya kuwa na ubaguzi wakijinsia kwaniNamtumbohaitakiwi kuwa kama ilivyo sasa” alisemaBw. Ngonyani.

No comments:

Post a Comment