Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Saturday 30 May 2015

TETEMEKO LA ARDHI LATIKISA JAPAN


Tetemeko kubwa la ardhi limetikisa mji wa Tokyo Japan.

Tetemeko hilo ambalo linakisiwa kuwa limefikia kipimo cha 7.8 kwenye vipimo vya Ritcher limetokea takriban kilomita 874 kutoka Tokyo kusini mwa Japan.
Kulingana na idara ya uchunguzi wa ardhi tetemeko hili lilitokea saa tano u nusu na lilidumu kwa takriban dakika moja.
Majengo mengi yalitikiswa mjini Tokyo.
Tetemeko la ardhi latikisa Japan
Hata hivyo hakuna taarifa zozote za uharibifu wala maafa kufikia sasa.
Kwa mujibu wa shirika la habari la taifa NHK kitengo cha kuzima moto mjini Tokyo wakaazi wa mji huo wamekuwa wakipiga simu kuomba msaada baada ya jamaa zao kujeruhiwa.
Shirika la habari la Reuters limesema kuwa huduma ya shirika la reli ya kuenda kasi ya Shinkansen imeathirika kwa muda baada ya kupotea kwa umeme.
Reli hiyo inahudumia miji ya Tokyo na Osaka.
Magari moshi mengine mjini Tokyo pia yamesimamishwa ilikuwaruhusu mafundi kukagua reli kama iliathirika au la.
Wasafiri wamesongamana nje ya vituo vya reli wakisubiri ruhusa ya kusafiri.
Wasafiri wamesongamana nje ya vituo vya reli wakisubiri ruhusa ya kusafiri.
Japan ni moja kati ya mataifa ambayo huathirika pakubwa na matetemeko ya ardhi.
Mwaka wa 2011,tetemeko kubwa lenye nguvu ya 9.0 katika vipimo vya Richter ilikisa taifa hilo na kutibua kimbunga kilichopelekea vifo vya zaidi ya watu elfu 20.
Aidha tetemeko hilo lilisababisha kuharibika kwa mitambo ya kuzalisha kawi ya kinyuklia ya Dai-Ichi katika mji wa Fukushima.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment