Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Saturday 30 May 2015

MAJESHI YAZIMA JARIBIO LA BOKO HARAM

Wanajeshi wazima shambulizi la Boko Haram Maiduguri
Jeshi la Nigeria limezima mashambulizi ya wapiganaji wa kiislamu wa Boko Haram katika mji wa Maiduguri ulioko Kaskazini Mashariki mwa taifa hilo.

Wapiganaji hao wa Kiislamu walikuwa wanafyatua makombora mazito mazito kuelekea mji huo usiku wa kuamkia leo lakini wanajeshi wakahimili mashambulizi na kuwakabili.
Watu 13 wameripotiwa kupoteza maisha yao katika mashambulizi hayo ya Boko Haram.
Rais Buhari ameapa kutokomeza kundi hilo la Boko Haram
Shambulizi limetokea saa chache baada ya kuapishwa kwa rais mpya wa Nigeria Jenerali mstaafu Muhammadu Buhari ambaaye ameahidi kukabiliana na tishio la mashambulizi ya kigaidi ya Boko Haram bila huruma.
Mwandishi wa BBC aliyeko Nigeria anasema kuwa huenda hii ni njia ya kundi hilo la wapiganaji kumuonesha Rais mpya kuwa wangali wapo licha ya mashambulizi makali dhidi yao na majeshi ya muungano wa mataifa ya Magharibi mwa Afrika.
Shambulizi limetokea siku moja tu tangu kuapishwa kwa Jenerali Buhari kuwa rais wa Nigeria
Rais Buhari akihutubia taifa punde baada ya kuapishwa alisema kuwa jeshi la taifa hilo litakita kambi yake katika mji huo wa Maiduguri ilikuitokomeza kabisa kundi hilo la waislamu la Boko Haram.
Awali Katika mahojiano maalumu na BBC, kiongozi huyo mstaafu wa jeshi amesema anatarajia kulishinda kundi hilo baada ya dhamira mpya kutoka jeshini na msaada wa nchi jirani.
"Kwa ushirikiano na majirani zetu Cameroon, Chad, Niger na jumuia ya kimataifa na dhamira ambayo tutapata kutoka katika jeshi, Nafikiri itachukua muda mfupi zaidi kukabiliana nao."
Mashambulizi ya Boko Haram yamewalazimisha raia wengi kutoroka makwao
Jenerali Buhari amesema tayari ameainisha msingi wa tatizo linalokabili nchi ya Nigeria, lakini amewataka raia wa nchi hiyo kuwa wavumilivu.
"Tumebaini matatizo makubwa matatu.
Ambayo ni kukosekana kwa usalama nchini, tatizo ambalo kila mmoja analifahamu na lingine ni ukosefu wa ajira, hii ina maana uharibifu wa uchumi ikiwa ni kutokana na vitendo vya rushwa na rushwa yenyewe.
Jenerali Buhari amesema tayari ameainisha msingi wa tatizo linalokabili nchi ya Nigeria, lakini amewataka raia wa nchi hiyo kuwa wavumilivu.
Matatizo haya matatu makuu, Wanigeria wote wanafahamu na tunaomba ushirikiano wa wananchi wa Nigeria,
wasitarajie miujiza kutokea katika kuyapatia ufumbuzi matatizo haya katika kipindi cha miezi michache baada ya kutwaa madaraka kwa sababu uharibifu umechukua miaka mingi,
miaka kumi na sita ya utawala wa chama tawala cha nchi hii." Anasema rais huyo mpya wa Nigeria.
CREDIT: BBC


No comments:

Post a Comment