Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Friday 15 July 2016

MALINZI AWAPONGEZA KUULI, NDULANE


Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amewapongeza Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi wa TFF, Wakili Revocatus Kuuli na Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Lindi, Francis Ndulane.


Kuuli, Wakili msomi aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Rufani ya Nidhamu ya TFF, ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Igunga mkoani Tabora.
Kadhalika, katika uteuzi huo huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli amemteua Ndulane ambaye ni Mjumbe Mkutano Mkuu wa TFF kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara mkoani Morogoro.
Katika salamu hizo, Rais Malinzi amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli kwa kuwateua viongozi hao wa TFF, akisema kwamba ameonyesha namna alivyo na imani na watendaji hao katika shughuli zao mbalimbali ikiwamo TFF.

No comments:

Post a Comment