Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Monday 16 May 2016

WANANCHI WAFUNGA BARABARA MKOANI MWANZA BAADA YA MTOTO KUGONGWA NA GARI

Wananchi na Wakazi wa Kata ya Kisesa, Wilaya ya Magu Mkoani Mwanza, mapema leo wamefunga barabara ya Mwanza-Musoma katika eneo la Kisesa na hivyo kusababisha abiria wanaoingia Jijini Mwanza kutoka Mikoani kukwama barabarani kwa zaidi ya saa moja.

Wamechukua maamuzi hayo baada ya dereva wa daladala moja kuwagonga wanafunzi wawili wa shule ya msingi Isangijo na kusababisha mmoja kufariki dunia papo hapo.

Baada ya hatua hiyo, jeshi la polisi, kikosi cha kuzuia ghasia limefika eneo la tukio na kuwasihi wananchi kufungua barabara hiyo ili kutowakwamisha abiria kuendelea na safari zao. 

Wananchi wakiwa wamefunga barabara ya Musoma-Mwanza, katika eneo la Kisesa baada ya daladala kuwagonga wanafunzi wa shule ya msingi Isangijo katika eneo hilo.

No comments:

Post a Comment