Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Saturday 14 May 2016

TAASISI ZA SERIKALI ZILIZOUNGANISHWA NA MFUMO WA SIMU ZENYE ITIFAKI YA INTANETI ZATAKIWA KUTUMIA HUDUMA HIYO KUPUNGUZA GHARAMA YA MAWASILIANO

 Mtaalamu TEHAMA, Bw. Dennis Elisha akiunganisha simu za 'IP phones' katika moja ya taasisi  za umma jijini Dar es salaam.

Na. Aron Msigwa – Dar es salaam.

Serikali kupitia Wakala ya Serikali Mtandao (e-Government Agency) imezitaka taasisi zote zilizounganishwa kwenye mfumo wa simu zenye itifaki ya intaneti (Internet Protocol (IP) ambazo zinatumia intaneti kuzitumia simu hizo katika mawasiliano yao kila siku ili kuboresha utendaji kazi na kupunguza gharama za mawasiliano Serikalini.Meneja  Habari, Elimu na Mawasiliano wa Wakala hiyo Bi. Suzan Mshakangoto amesema  kuwa Serikali imeamua kusisitiza matumizi ya simu hizo ili kuziwezesha taasisi  za Serikali kuwa na mawasiliano yaliyo bora, salama na kupunguza gharama za mawasiliano.

Amesema kuwa Serikali kupitia Wakala ya Serikali Mtandao (eGA) imeunganisha taasisi za  Serikali 72 ambazo zinajumuisha Wizara, Idara  zina zojitegemeana na Wakala za Serikali na kuongeza kuwa taasisi hizo zimeunganishwa na Mtandao wa Mawasiliano wa Serikali yaani Government Communication Network (Govnet)’ unaowezesha mfumo wasimu hizo kufanya kazi kwa ufanisi.

  Kupitia mfumo wa simu hizi zenye itifaki ya intaneti mtumishi wa taasisi  iliyounganishwa anaweza kupiga simu kwenda taasisi nyingine ya nje ikawa kama amepiga simu ya ‘extension’ ndani ya ofisi moja Amesema Bi. Suzan.

Aidha, amesema Taasisi za umma zitanufaika moja kwa moja na simu hizo kwa kuwa, taasisi hizo zitaweza kubadilisha na taarifa kupitia mtandao mmoja tuwa Mawasiliano wa Serikali kwa usalama na uhakika. Pia simu hizo zitawawezesha watumishi wa taasisi mbalimbali kufanya mkutano kwa njia ya simu wakiwa kwenye ofisi zao na hivyo kuokoa muda na gharama za usafiri.

Hata hivyo amesema taasisi za umma zilizopo katika mtandao wamawasiliano wa Seikali zitaendelea kuwasilia na na taasisi zilizo nje ya mtandao huo kwa kupitia mtoa huduma wa simu za mezani (PSTN Provider) kama vile TTCL.



No comments:

Post a Comment