Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Thursday 27 August 2015

MISRI YAJITOA MICHEZO YA AFRIKA

Nchi ya Misri imetangaza kujiondoa dakika za mwisho kushiriki kwenye fainali za Michezo ya Afrika (All Africa Games) kwa timu zake za Wanawake na Wanaume, fainali zinazotarajiwa kuanza kutimu vumbi mwezi Septemba nchini Congo- Brazzavile.
Kwa mujibu wa kifungu cha 19 (B) cha uendeshaji wa michuano hiyo kinasema “Kama timu itajiondoa baada ya kuwa imeshafuzu kwa hatua ya fainali, lakini kabla ya kuanza kwa michezo yenyewe, Kamati ya Uendeshaji wa Mashindano itaziba nafasi hiyo kwa kuteua timu iliyotolewa katika hatua ya mwisho”.
Kujitoa kwa timu za wanawake na wanaume za Misri, kunatoa nafasi kwa Kamati ya Uendeshaji wa Mashindano kuzipa nafasi timu za Senegali (Wanawake), na Burundi (Wanaume) ambazo zilitolewa na Misri katika hatua ya mwisho.
Misri ilipangwa katika kundi B kwa Wanawake na timu za Cameroon, Ghana na Afrika Kusini, huku timu ya Wanaume ikiwa kundi B na timu za Ghana, Senegal na Nigeria
Wakati huo huo Mwamuzi Ferdinand Chacha kutoka Tanznaia ameteuliwa kuwa miongoni wa waamuzi wa michuano ya Michezo ya Afrika (All Africa Games) nchini Congo-Brazzavile.
TFF inampongeza Chacha na kumtakia kila la kheri katika kuipeperusha bendera ya Tanzania katika michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment