Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Thursday, 4 June 2015

GOOGLE YAMUORODHESHA MODI KAMA MHALIFU

Waziri Mkuu wa India, Naendra Modi
Kampuni ya mtandao wa Google imeomba radhi baada ya picha za waziri mkuu wa India Narendra Modi kuonekana katika picha za watu kumi wahalifu.

''Tunaomba radhi kwa kuchanganyikiwa na kutoelewana ambako kumesababishwa na picha hizo'',taarifa iliotoka kwa kampuni hiyo ilisema.
Picha za Modi zinaonekana unapowatafuta watu 10 wahalifu pamoja na magaidi,wauaji na madikteta.
kampuni ya mtandao wa Google
Viongozi wengine duniani waliomo katika orodha hiyo ni aliyekuwa rais wa Marekani George Bush na Libya Muammar Gaddafi.
Viongozi wengine wakuu wanaopatikana ni waziri mkuu wa Delhi Arvind Kejriwal,wakili Ram Jethmalani na mtoro Dawood Ibrahim pamoja na mwigizaji wa Bollywood Sanjay Dutt ambaye kwa sasa anahudumia kifungo kutokana na mlipuko mkubwa uliotokea mjini Mumbai mwaka 1993.
''Haya matokeo yanatushangaza na hayawakilishi maoni ya Google'',kampuni hiyo ilisema katika taarifa yake iliotolewa Jumatano usiku.
Waziri mkuu wa India Narendra Modi na rRis Obama
Kampuni hiyo imesema kuwa matokeo hayo yanatokana na gazeti moja la Uingereza ambalo lilichapisha picha ya Modi kimakosa.
Msamaha huo unajiri baada ya wanasiasa wengi wa India kuonyesha wasiwasi wao katika mitandao ya kijamii.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment