Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Sunday 28 June 2015

WATU 15 KATI YA WALIOUAWA TUNISIA NI WAINGEREZA


Maelfu ya watalii wanaondoka Tunisia baada ya shambulio katika hoteli ya watalii iliyosababisha vifo vya watu 38 wengi wao wazungu.

Makampuni ya utalii pia yanavunja safari za kwenda huko.
Katika uwanja wa ndege wa Hammamet, karibu na Tunis, watalii wamepanga foleni kusubiri kuondoka nchini humo.
Serikali ya Tunisia inasema kuwa ulinzi umezidishwa katika maeneo ya utalii huku wanajeshi wa akiba wakitakiwa kuripoti kazini mara moja.
null
15 kati ya waliouawa Tunisia ni Waingereza
Aidha serikali imetangaza kuwa itafunga misikiti 80, inayodaiwa kuwa inafundisha utumizi wa nguvu na Jihad.
Islamic State imesema imehusika na shambulio hilo.
Mshambuliaji aliyekuwa na bunduki, baadae alipigwa risasi na kuuawa.
null
Maelfu ya watalii wanatoroka Tunisia kufuatia shambulizi la kigaidi
Wakati huo huo inaaminika sasa kuwa 15 kati ya wale waliouawa huko Tunisia ni raia wa Uingereza.
Waziri mkuu wa Uingereza, David Cameron, amesema shambulio hilo ni kumbusho la kikatili na kusitikisha, kwamba kuna tisho la ugaidi dunia nzima
"Nitahakikisha, tunafanya tuwezalo kusaidia, na kuwakinga watu na mashambulio ya kigaidi''.
null
Maelfu ya watalii wanatoroka Tunisia kufuatia shambulizi la kigaidi
''Tunawakumbuka na kuwaombea waliofiwa, na wale waliojeruhiwa''.
''Tunashirikiana na wakuu wa Tunisia, kujua idadi kamili ya Waingereza waliouliwa.''
Lakini wananchi wa Uingereza wanafaa kujitayarisha, kuwa wengi waliouwawa ni Wangereza."Alisema Cameroon.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment