Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Friday 26 June 2015

ALIOA SIKU TATU TU KABLA YA KUFARIKI DUNIA


Kijana mmoja barubaru alimuoa mpenzi wake siku tatu tu kabla yake kuaga dunia kutokana na Saratani ya damu lukaemia.

Omar Al Shaikh alimuoa mpenzi wake Amie Cresswell, wote wenye umri wa miaka 16, katika wadi ya hospitali kuu ya Malkia Elizabeth ilioko Birmingham Uingereza.
Omar, aliaga dunia Jumatatu hii siku tatu tu baada ya kufunga pingu za maisha na Amie.
Omar aliaga dunia baada ya kukosa mtu ambaye damu yake inayoingiana na yake.
Omar alimchumbia Amie baada ya kufahamishwa na madaktari kuwa alikuwa na siku 5 tu za kuishi.
Mamake bi Mirabela anasema kuwa alijizatiti hadi siku yake ya mwisho.
''amejikaza sana na kupanga kila kitu alichotaka kifanyike''alisema mamake
null
Omar aliaga dunia baada ya kukosa mtu ambaye damu yake inayoingiana na yake
"alitaka sana kumuoa Amie,alikuwa akinieleza kuwa angefurahia sana akisimama mbele ya haki na kumweleza mwenyezi mungu kuwa Amie alikuwa ni mkewe''
Shangazi yake Anca Dumitriu alisema "Ilikuwa ni siku nzuri sana kwani wote walifurahia sana''
Omar alimwambia Amie ''Wewe ni mke wangu sasa''
Mwanajeshi huyo mtarajiwa Omar, aligunduliwa kuwa anaugua Lukemia baada ya kuanguka na kuzirai alipokuwa akicheza mpira.
Kutokana na asili yake ya Kirumi na Kiarabu ilikuwa vigumu sana kupata mtu mwenye chembechembe zitakazoingiana.
Mamake alisema tangu afahamishwe kuhusu kuzoroteka kwa hali yake ya siha mapema mwezi huu Omar amejitahidi kuwa mchangamfu hadi alipoaga dunia.
''Aliaga dunia usingizini.''
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment