Mkurugenzi wa chuo cha Musoma utalii
Shaban Mrutu
Sehemu ya mbele ya jengo la Chuo cha
Musoma Utalii. (Picha zote na Hastin Liumba)
Na Hastin Liumba, Tabora
UMASIKINI ni kitu ambacho siku zote kimekuwa kikikwamisha mambo mengi miongoni mwa jamii nchini.
UMASIKINI ni kitu ambacho siku zote kimekuwa kikikwamisha mambo mengi miongoni mwa jamii nchini.
Hali hiyo imekuwa ni kikwazo cha kufikiwa
kwa malengo yanayokusidiwa katika mikakati ya maendeleo tarajiwa. Lakini
maendeleo hayawezi kuja kirahisi bila ya jamii kupata elimu bora.
Wengi wa wazazi na walezi wameshindwa kusomesha watoto kutokana na kukosa uwezo wa kusomesha na hali hiyo imesababisha kaya nyingi kuwa masikini.
Wengi wa wazazi na walezi wameshindwa kusomesha watoto kutokana na kukosa uwezo wa kusomesha na hali hiyo imesababisha kaya nyingi kuwa masikini.
Mkurugenzi wa chuo cha Musoma Utalii
mkoani Tabora Shaban Mrutu alisema hayo wakati akifanya mahojiano na mwandishi wa
makala hii.
Mrutu alisema kwa kutambua umuhimu wa
elimu katika jamii alianzisha mpango wa kusomesha watoto yatima, watoto
waishio kwenye mazingira magumu na wasiojiweza.
Alisema chuo kimekuwa na mfuko maalumu wa
kusomesha watoto hao kwa mpangilio ulio bora ambao utashirikisha serikali na
wadau wa elimu, mpango huu ulianza mwezi Januari 2014.
Alibainisha watoto hao wanachukuliwa
wakiwa na sifa maalumu za kujiunga na vyuo na watachukuliwa watoto wanne kila
muhula.
Alibainiaha masomo watakayochukua ni yale
ambayo yanayofundishwa chuoni hapo na kozi hizo zitaendana na sifa ya mtoto
atayechukuliwa.
Kozi zitolewazo chuoni
Aidha mkurugenzi huyo alitaja chuo
kinatoa kozi wanazotoa kuwa ni Tour Guide and Administration, Tourism and Airline
Management, Travel Studies and Tour Operation.
Alitaja nyingine ni International Hotel
Managemet, Food and Beverage Services and Sales, Food Production Cooker and Bakery,
Front Office Operation, Information
and Communication Technology (ICT).
Mrutu anaongeza kozi nyingine ni Nurcsery
School Teacher (Early Childhood Education), Journalism Radio and TV Broadcasting),Secretarial
Course, Records Management, Procurement and Supply Management na
Business Administration na kozi hizi ni kwanga ngazi ya Cheti (NTA Level 4).
Business Administration na kozi hizi ni kwanga ngazi ya Cheti (NTA Level 4).
Aidha aliongeza zipo kozi fupi za Computer
in office Application,
Computer Maintenance and Electronics, Computer Knowledge na Graphic and
Disegn.
Nyingine ni Music Prodactions, Elementary/ foundation Course, Entrepreneurship
Development na English, French and Italian.
Mrutu alibainisha kuwa chuo pia kinatoa
kozi ngazi ya Diploma (NTA) Level 5 &6 Tour Guiding and
Administration,Imformation Communication Technology,Early Childhood care
and Education, Journalism, Radio& TV Broadcasting, Hotel Management,
Business Administration, Records Management, Full Secretarial Course na
Diploma in Primary School Education.
Mrutu alibainisha mpango huo wa kusomesha
watoto wasiojiweza unahusisha
mwanafunzi anayekubali kuishi bweni ama kutwa na atalipiwa gharama zote.
Vigezo vitakavyotumika
Mrutu anasema mtoto atapatikana kwa
kupitia vigezo vitakavyowekwa ambavyo ni barua za utambulisho toka kwa mwenyekiti wa
mtaa,kitongoji,kijiji na mkuu wa wilaya.
Alisema hadi sasa chuo kimeshachukua
watoto wanne ambao wanaendelea na masomo hadi sasa na maendeleo yao ni mazuri.
“Nimeamua kusomesha watoto hawa kwa
kutambua umuhimu wa elimu hasa katika kipindi hiki cha mabadiliko makubwa ya Sayansi
na Teknolojia duniani.”aliongeza.
Alisema hatua hiyo ina lengo la kusaidia
watoto wenye nia na dhamira ya kusoma lakini hawana uwezo wa kupata fursa hiyo
hasa kutokana na wazazi na walezi kuwa na hali duni.
Changamoto anazokumbana nazo
Mrutu anasema licha ya mpango kuwenda
vyema bado amekuwa akikumbana na changamoto kadhaa ambazo ni baadhi ya vijana wanaokuja
wanakosa sifa na vigezo.
Alitaja nyingine ni idadi ya vijana
wanaokuja inakuwa kubwa kuliko uwezo wa mfuko wa kusomesha watoto hao huku wengine
wakigushi barua toka kwa wenyeviti wa mitaa,vitongoji na vijiji.
Licha ya hayo amekuwa akifatilia kwa
ukaribu ili watoto waliolengwa wanachukuliwa na siyo kuchukua watoto
wasiokuwa kwenye mpango.
Aidha alishauri viongozi ngazi za
mtaa,vitongoji na vijiji wasitumike vibaya kubaini watoto wanaowapa
barua za kutambulisha kama familia haina uwezo.
Malengo ya mpango huo
Mrutu anasema malengo ya mpango huo
alioanzisha ni kutafuta wafadhili ili kuweza kuchukua idadi ya watoto
wengi wenye uhitaji.
Alisema anakusudia kuboreha mfuko huo ili
kuweza kuchukua watoto 10 kila muhula lakini kabainisha anahitaji
kuungwa mkono na wadau,serikali na wafadhili kufanikisha hilo.
Alisema uwepo wa chuo hiki kanda ya
magharibi kutasaidia watumishi sekta ya utalii katika maeneo mbalimbali
kanda hii kuendelea kupata elimu bora na kuboresha huduma kwa wananchi.
Mrutu anasema mpango huo wa chuo ni
sehemu ya utekelezaji wa ilani ya serikali ya CCM pamoja na mambo
mengine inatilia mkazo upatikanaji wa elimu bora mkoani Tabora na kwa
watanzania wote.
Alibainisha malengo mengine ni watoto
watakaofanya vyema na kufaulu vizuri masomo yao watasaidiwa kutafutiwa
ajira.
Alisema ufaulu wa wanafunzi siyo suala la
mwalimu na mwanafunzi pekee bali ni wajibu wa jami nzima.
Mkurugenzi huyo anasema jamii inakuwa na wajibu wa kusaidia maeneo mbalimbali hususani upatikanaji wa mazingira bora ya kujifunzia na kufundishia.
Mkurugenzi huyo anasema jamii inakuwa na wajibu wa kusaidia maeneo mbalimbali hususani upatikanaji wa mazingira bora ya kujifunzia na kufundishia.
Alibainisha mpango huo umelenga pia
utekelezaji wa mpango wa matokeo makubwa sasa (BRN) pamoja na
kutathimini utekelezaji wa mkakati.
Wito kwa jamii
Wito kwa jamii
Mkurugenzi huyo anatoa wito kwa jamii,
wafadhili, wadau wa elimu na serikali kusapoti mpango wake ili kunusuru
watoto ambao wana nia ya kusoma lakini wanakosa haki hiyo kwa kutokuwa
na uwezo wa kifedha.
“Kundi hili la watoto wasiojiweza ni
kubwa nchini hivyo ninahitaji kujipanga zaidi na hili linawezekana hata
kwa taasisi nyingine kama yangu tujitoe tu.” aliongeza.
Alisema anaiomba serikali kuunga mkono
hatua hiyo kwani itasaidiwa vijana ambao wana sifa na uhitaji wa elimu
kushindwa kufikia malengo yao.
hastinliumba@gmail.com-
No comments:
Post a Comment