Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Thursday 26 March 2015

UZINDUZI WA USHIRIKA WA JITIHADA NJEMA ZANZIBAR

Dr Ali Mohamed Shein


Dk. Ali Mohamed Shein, Rais wa Zanzibar

Na Miza Othman, Maelezo-Zanzibar
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinbuzi  Mhe. Ali Mohamed Shein amesema kuanzishwa kwa vikundi vya ushirika (SACCOS) ni njia moja ya kujiimarisha kiuchumi na kupambana na umasikini Visiwani Zanzibar.
Ameyaeleza hayo katika hafla ya uzinduzi wa Ushirika wa Jitihada Njema wa Bandari  ya Zanzibar huko ukumbi wa Hoteli ya Bwawani mjini Zanzibar.
Amesema uanzishwaji  wa vikundi vya ushirika hasa wa vijana na kinamama, ni njia ya kuendesha maeneo maalumu ya kufanyia shughuli zao za Biashara ndogondogo pamoja na kuzitambua rasilimali ambazo ziko kwenye sekta zisizo rasmi vikiwemo vikundi hivyo.
 Dr. Shein amesema lengo la Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, ya awamu ya saba ambayo azma yao ni kuviimarisha vikundi vya ushirika vinavyokwenda sambamba na ilani ya uchaguzi Mkuu ya Chama cha CCM ya Mwaka 2010 ambalo amelibainisha wakati alipozinduwa Baraza la nne la Wawakilishi  tarehe 11 Novemba 2010 katika hutuba yake ya uzinduzi huo.
Aidha ameeleza kuwa kufanya hivyo ni kuimarisha Mfuko wa Uwezeshaji wa wananchi kiuchumi ili kukuza uwezo wa kutowa mikopo kwa wananchi na kuwawezesha kutumia fursa zilizopo katika maeneo yao.
Hata hivyo amesema Serikali itashirikiana nao katika kuzitafutia ufumbuzi changamoto zinazowakabili ili waweze kupata ufanisi zaidi wa kuendeleza vikundi vyao.
Wakiwasilisha risala yao wana kikundi cha ushirika wa Jitihada Njema wameliomba Shirika la Bandari la Zanzibar kuwapatia kiwanja ili waweze kujenga ofisi yao kwa lengo la kukiendeleza kikundi chao.
Pia wamesema kwamba lengo la Ushirika wao ni kuwapatia mikopo wananchi, kuutangaza ushirika wao ndani ya jamii ili kuwatengenezea  ajira vijana, kutatuwa changamoto zinazowakabili wanaushirika hao, kusaidia kujuwa mbinu mbalimbali za elimu na kuwarahisishia upatikanaji wa Bima ya Afya.
Hata hivyo wamesema tatizo kubwa kwa sasa linalowakabili katika kikundi cha ushirika wao  ni ukosefu wa ofisi  yenye eneo la kutosha kwa ajili ya shughuli zao jambo ambalo linawarejesha nyuma kwa kiasi kikubwa katika utendaji wao  kazi.
Ushirika huo ulianzishwa tarehe 31 Januari, 2004 ikiwa na wanachama 100 na hadi sasa una wanachama 200 na tayari wameshafunga mkataba wa kupatiwa mikopo na Shirika la Bandari.

No comments:

Post a Comment