Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Sunday, 7 June 2015

KUMBUKUMBU ZANGU: MAULIDI DILUNGA AFUNGIWA MIAKA MIWILI KWA KUTOROKA KAMBINI

Maulid Dilunga
Na Daniel Mbega
Zamani kulikuwa hakuna ustaa wala nini katika suala la maamuzi, tofauti na sasa ambapo wachezaji wakisifiwa kidogo wanavimba vichwa na kujiona bila wao timu haziwezi kufanya vizuri.
Ikitokea mamlaka husika zikachukua hatua, basi utawaona mashabiki wakishika bango na kuwatetea wachezaji hao bila kutambua kwamba nidhamu ndio msingi wa mafanikio katika michezo. Mashabiki wanaweza kuwatukana makocha na viongozi na siyo ajabu wakiwasingizia kwamba ‘huenda wamenyang’anyana mademu’ mitaani ndiyo maana kocha ama kiongozi anamchukia mchezaji husika.
Utoro katika kambi za timu zetu limekuwa jambo la kawaida siku hizi, ulevi na uvutaji wa bangi ni mambo yaliyotawala, lakini zamani haikuwa hivyo. Zamani hawakujali umaarufu wako wala nini, sheria ilikuwa msumeno.
Mnamo Desemba 21, 1971 Mkutano wa Chama cha Soka Tanzania (FAT) na kile cha Zanzibar (ZFA) uliofanyika Unguja uliamua kumfungia kucheza soka miaka miwili mshambuliaji wa Yanga na Taifa Stars Maulid Bakari Dilunga kutokana na utovu wa nidhamu.
Ilielezwa kwamba, Dilunga alitoroka kwenye kambi ya timu hiyo iliyokuwa Jeshi la Wokovu na kwenda kulewa na kucheza disko kwa siku mbili, na hivyo siku timu ya taifa ilipoondoka kwenda Guinea kwa mechi za kirafiki hapo Novemba yeye hakuwepo.
Ikiwa huko Guinea, Tanzania ilipoteza mechi zake zote mbili ambapo mechi ya kwanza ilichezwa Novemba 2, 1971 mjini Conakry na wenyeji wakashinda kwa mabao 4-2.
Ziliporudiana tena mjini humo Novemba 14, 971 Guinea ikapunguza dozi na kuifunga Tanzania mabao 3-2.
Baadaye adhabu hiyo ikapunguzwa na Dilunga akarejea uwanjani, hasa baada ya yeye mwenyewe kuomba radhi.


0656-331974

No comments:

Post a Comment