Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Friday, 12 June 2015

ALIYEPACHIKWA UUME, SASA BABA MTARAJIWA

Madaktari wakiwa katika chumba cha upasuaji
Daktari wa usapuaji nchini Afrika Kusini amethibitisha kwamba mwanamme wa kwanza aliyepandikizwa uume atakuwa baba hivi karibuni.

Professor Andre van der Merwe, ambaye ndiye aliyefanya upasuaji huo mwezi Disemba, ameiambia BBC kwamba mwenza wa mgonjwa huyo ana uja uzito wa miezi minne.
Mwanamme huyo mwenye umri wa miaka 21 alipoteza uume wake pindi alipokuwa anapashwa tohara ambayo haikufanikiwa.
Professor van der Merwe ameendelea kusema habari hizo zinaonyesha kuwa upandikizwaji huo wa kiungo umefanikiwa kabisa na unaweza kufanyiwa wagonjwa wengine katika siku zijazo.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment